TANGAZO


Thursday, March 10, 2016

BAKITA wahaswa kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura akizungumza na Katibu Mtendaji BAKITA (hayupo pichani) alipotembelea ofisi za Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam.(Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo)

Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Selemani Sewange (katikati) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (kushoto) alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Kulia ni maafisa Utamaduni kutoka Wizara hiyo.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (kushoto) akipokea Kamusi Kuu ya Kiswahili kutoka kwa Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Selemani Sewange alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (kushoto) akikabidhiwa kitabu kiitwacho Furahia Kiswahili kilichoandaliwa na BAKITA alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Anayemkabidhi ni Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Seleman Sewange.


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura akipitia Kamusi kuu ya Kiswahili aliyopewa baada ya kutembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam.


Mtaalamu kutoka Idara ya Istilahi na Kamusi Taasisi ya BAKITA Bw. Mayolwa John (kushoto) akimwelezea Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (kulia) kazi zinazofanywa na Idara hiyo alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Selemani Sewange.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (wapili kushoto) akiangalia mfumo wa mradi wa kukuza kiswahili katika kompyuta ulioandaliwa na BAKITA alipotembelea Taasisi hiyo kufahamu mambo mbalimbali wanayoyafanya jana jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dr. Selemani Sewange na kushoto ni Afisa Utamaduni Bw. Christopher Mhongole. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (wapili kulia) akiongea na wataalamu wa Lugha na Fasihi kutoka Taasisi ya BAKITA alipotembelea Taasisi hiyo kufahamu mambo mbalimbali wanayoyafanya jana jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Seleman Sewange.

Na Genofeva Matemu -Maelezo
Tarehe: 10/03/2016
WATENDAJI Taasisi ya Kiswahili Taifa (BAKITA) wametakiwa kijitangaza na kushiriki katika matukio mbalimbali ya kitaifa na kimataifa kuhamasisha matumizi la lugha ya Kiswahili ili kiweze kufahamika na kutumika na mataifa mengine.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Wazari wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura alipotembelea ofisi za BAKITA kutambua kazi mbalimbali zinazofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam.

“Ni vyema kama mtakua mkiomba nafasi ya kushiriki katika matukio yote yanayofanyika ndani na nje ya nchi ili muweze kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili kwani ni lugha ambayo inakua kwa kasi na kutumiwa na watu mbalimbali” alisema Mhe. Wambura.

Akizungumza wakati wa ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dr. Selemani Sewange amesema kuwa BAKITA imekua ikishiriki katika Bunge la Afrika na Umoja wa Afrika hivyo kutangaza lugha ya kiswahili kwa mataifa mengine na kuahidi kuendelea kushiriki katika fursa zote zitakazojitokeza ndani na nje ya nchi.

Aidha Dr. Sewangi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa kuitanganza nchi na lugha ya Kiswahili alipokutana na marais wa Afrika Mashariki hivi karibuni Mkoani Arusha. 

“Lugha ya Kiswahili itafahamika na kutumika na watu wa mataifa mengine kama itatumiwa na wazalendo katika matukio ya kimataifa kama alivyofanya Mhe. Magufuli alivyokutana na Marais wa Afrika Mashariki hivi karibuni” alisema Dr. Sewange.

Baraza la Kiswahili la Taifa ni Taasisi iliyo chini ya Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo iliyoundwa chini ya sheria namba 27 ya Bunge la mwaka 1967 kukuza na kuendeleza matumizi ya Lugha ya Kiswahili  Tanzania, kukuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili katika shughuli rasmi na za umma, kuleta mafanikio makubwa katika matumizi ya Lugha ya Kiswahili na kukataza matumizi mabovu.

No comments:

Post a Comment