Nico Rosberg alipata ushindi wake wa kwanza kabisa katika muda wa miezi minne baada ya kumshinda mwenzake wa Mercedes Lewis Hamilton katika mashindano ya magari yaendayo kasi ya Mexican Grand Prix.
Mjerumani huyo alidhibiti mbio hizo kuanzia mwanzo, bingwa mpya wa dunia Hamilton akimfuata unyounyo lakini hakuweza kumpita.
Ushindi huo wa Rosberg, ambao ndio wake wa nne msimu huu, umemrejesha katika nambari mbili kwenye kinyang’anyiro cha kusaka ubingwa akiwa nyuma ya Sebastian Vettel wa Ferrari ambaye hakuweza kumaliza mbio hizo.
Valtteri Bottas wa Williams anashikilia nafasi ya tatu.
Tukio la kusisimua kwenye mbio hizo lilikuwa ni uhasama uliotarajiwa kwenye kambi ya Mercedes kati ya Rosberg na Hamilton.
Timu hiyo ilikuwa imeamua kutua mara moja pekee lakini wakiwa wamesalia na mizunguko 25 kati ya mizunguko 71 waliyokuwa wakikimbia, Mercedes walimtaka Rosberg kusimama mara ya pili.
Mzunguko uliofauata walimtaka Hamilton pia asimame.
Hamilton alipinga ombi la hilo lakini mwishowe hakuwa na budi kwani aliambiwa lilikuwa “agizo” kwa sababu za kiusalama.
No comments:
Post a Comment