Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren (kushoto) akitoa hotuba yake wakati wa mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.(Katikati) ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Anjelina Madete na Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira kutoka ofisi hiyo, Joseph Kihaule.
Picha ya pamoja kati ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Anjelina Madete (wa pili kushoto) mara baada ya kufungua mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira kutoka ofisi hiyo, Joseph Kihaule na (wa pili kulia) ni Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti (UNITAR), Carlos Maren. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa mazingira kutoka ofisi hiyo, Rogathe Kisanga.
Issaria Mangalili akitoa mada juu ya mikataba mbalimbali inayohusu kemikali mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Issaria Mangalili akitoa mada juu ya mikataba mbalimbali inayohusu kemikali mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Joseph Kihaule (kushoto) akisisitiza jambo wakati akiongoza mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam, kulia ni Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren.
Wadau wa mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana wakijadiliana jambo kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Na Magreth Kinabo- Maelezo
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Anjelina Madete (katikati) akifungua mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira kutoka ofisi hiyo, Joseph Kihaule na kushotoni Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Anjelina Madete(katikati) akifungua mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira kutoka ofisi hiyo, Joseph Kihaule na kushotoni Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren.
Issaria Mangalili akitoa mada juu ya mikataba mbalimbali inayohusu kemikali mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Issaria Mangalili akitoa mada juu ya mikataba mbalimbali inayohusu kemikali mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Joseph Kihaule (kushoto) akisisitiza jambo wakati akiongoza mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam, kulia ni Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren.
Wadau wa mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki uliofanyika jana wakijadiliana jambo kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
Mdau wa mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya Zebeki uliofanyika jana kwenye hoteli ya peacock jijini Dares Salaam, Anne Sekiete ,ambaye ni Afisa Afya Mkuu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akichangia jambo. Picha zote na Magreth Kinabo – Maelezo
Na Magreth Kinabo- Maelezo
JAMII imelezwa kwamba ulaji wa samaki wakubwa na vyakula vya jamii hiyo(shellfish),ambao wameathirika madini ya zebaki kwa wingi unasababisha binadamu kupata madhara ya kiafya kutokana na baadhi ya samaki hao kula samaki wadogo wenye madini hayo.
Samaki hao huathirika na madini hayo kutokana na shughuli za mlipuko wa volkano, mmomonyoko wa ardhi, na shughuli za kibinadamu ambazo ni uchimbaji mdogo wa madini,uchomaji wa mkaa, uzalishaji wa saruji.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Anjelina Madete wakati akifungua Mkutano wa Mkataba wa Minamata kuhusu madini ya zebaki, ambayo ulijadili juu ya mbinu za utekelezaji wake ili kuweza kuepusha madhara kwa jamii uliofanyika jana kwenye hoteli ya Peacock jijini Dares Salaam.
“Watu huathiriwa na madini haya katika mazingira tofauti, ingawa huathiriwa zaidi kutokana ulaji wa samaki ambao wana madini haya na pia kwa kuvuta hewa yenye madini haya kutokana na shughuli za viwandani,” alisema.
Aliyataja makundi ambayo ni rahisi kupata madhara ya madini hayo kuwa ni watoto wachanga ambao hawajazaliwa kutokana mama zao kutumia vyakula vya jamii hiyo, hali inayosababisha kuathiri ukuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu kwa watoto, hivyo huathiri uwezo wa kufikiri, kumbukumbu , uelewa, kuwa na umbo dogo na uwezo wa kuona.
Aliongeza kuwa, kundi la pili linaloathirika kuwepo kwa madini hayo kwa wingi ni jamii inayoishi kwa kutegemea samaki uchunguzi umeonyesha 1.5/1000 na 17/1000 watoto waliopata upungufu wa akili kutokana na matumizi ya samaki wenye madini hayo katika nchi za Brazil ,Canada, China, Columbia na nchi za ukanda wa kijani.
Naibu Katibu Mkuu huyo pia aliyataja madhara yanayotokana na kuwepo kwa madini ya zebaki mwilini kwa wingi ni huathiri kwa mfumo wa fahamu, usagaji wa chakula, kinga za mwili mapafu, figo, ngozi na macho.
Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizosaini Mkataba huo Oktoba 10 nchini Japan mwaka 2013. Hivyo elimu inahitajika kwa jamii juu madini hayo ikiwemo kujenga uwezo wa rasilimali watu, miundombinu na mahitaji mengine kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa upunguzaji wa madini hayo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti(UNITAR), Carlos Maren alisema wamefurahishwa na kitendo cha Tanzania kuweka mikakati ya utekelezaji wa mkataba huo ili kuokoa maisha ya watu, hivyo wataendelea kutoa ushirikiano.

No comments:
Post a Comment