TANGAZO


Monday, June 15, 2015

EWURA yapata Tuzo ya Mdhibiti Bora

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati  na Maji (EWURA), Bw. Felix Ngamlagosi, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari  leo kuhusu kitabu cha mikataba ya kuuziana umeme ambacho alishiki kukiandika. Kulia ni Mkurugenzi wa Umeme kutoka  Mamlaka ya Udhibiti wa  Huduma za Nishati  na Maji (EWURA), Anastas Mbawalla. 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati  na Maji (EWURA)  Bw. Felix Ngamlagosi (kushoto) akionesha tuzo  ya  mdhibiti bora  wa mwaka wa nishati  iliyotolewa kwa mamlaka hiyo  na Jukwaa la Nishati  Afrika  wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Umeme kutoka mamlaka hiyo, Anastas Mbawalla.

Mkurugenzi wa Umeme kutoka mamlaka hiyo, Anastas Mbawalla (kulia), akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa  Huduma za Nishati  na Maji (EWURA),  Bw. Felix Ngamlagosi. (Picha na Salma  Ngwilizi –Maelezo)

Na Magreth Kinabo- maelezo
MAMLAKA ya Udhibiti wa  Huduma za Nishati  na Maji (EWURA) imebuka  mshindi wa mashindano ya Tuzo ya Mdhibiti Bora wa mwaka wa Nishati ya 2015.

 Hayo yalisemwa  leo  na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Bw. Felix Ngamlagosi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu tuzo hiyo iliyotolewa na Jukwaa la  Nishati la Afrika.

 Tuzo hiyo ambayo ilitolewa Juni 8, mwaka huu kwenye sherehe   ya mkutano mkuu wa kila mwaka uliofanyika   Juni 8 hadi 11 mwaka huu Dubai,Umoja wa Falme za Kiarabu.

 “Jopo la wataalamu  la wanaofanya kazi kwa kushirikiana na  shirika la  EnergyNet  la  Uingereza lilikaa na kuchagua   EWURA   kuwa ndio mshindi wa kwanza wa mwaka 2015 katika kundi la wadhibiti,’’ alisema Ngamlagosi.

 Ngamlagosi   alisema tuzo hiyo ni ya mara ya kwanza kutolewa  nchini  imepatikana baada jopo hilo kuangalia vigezo vya   kufanya kazi vizuri, kutoa maelekezo kwa wadau kwa ufasaha bila mabadiliko, na kueleweka kwa wadau. Pia mamlaka hiyo imeandaa kanuni  mbalimbali ambazo ni za uzalishaji na uuzaji umeme, usafirishaji umeme na kusambaza umeme zikiwemo leseni.

 Aliongeza kwamba tuzo hiyo inafanya Tanzania kutambulika kimataifa  kama ni nchi  yenye  taasisi thabiti ya uhakika ya udhibiti wa sekta ya nishati na maji ambalo ni jambo muhimu kwa nchi kuendelea kuimarisha wawe

Alisema Tanzania sasa itashuhudia upatikanaji wa kiwango cha juu  cha   mitaji ya uwekezaji  kutoka nje ya nchi (FDIs)kwenye sekta za nishati na maji ,ambazo zitavutia uwekezaji zaidi kwenye sekta zingine kwa kuzingatia kutegemeana kwa sekta kati ya sekta ya nishati zingine kiuchumi.

 Hivyo Tanzania ipata wawekezaji wa umeme mijini na vijijini kutokana na kuwepo kwa mfumo imara na uwazi unaoleweka  katika sekta hiyo.

 Ngamlagosi alizitaja taasisi zingine zilizoshirikia kwenye shindano hilo ni Mamlaka ya Udhibiti wa Umeme Cameroon(AESEL) Kamisheni ya Udhibiti wa Umeme na Maji ya Mali (CREE) Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati ya Uganda(ERA)na   Kamisheni ya  Udhibiti wa Nishati ya Kenya(ERC). 

Aliongeza kuwa Tanzania ilishiriki kuandika kitabu cha mikataba ya kuuziana umeme, ambapo Mkurugenzi wa Umeme , Anastas Mbawalla alishiriki pamoja na japo la wataalamu, ambacho kinatarajiwa kuzinduliwa mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.

No comments:

Post a Comment