TANGAZO


Monday, June 15, 2015

Ataka wanasiasa kusaidia watoto waishio katika mazingira magumu

 Kampeni Meneja wa ujenzi wa  Kituo cha New Hope Family Group, Braiton Balige akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujenzi wa kituo hicho. (Picha zote na Salma Ngwilizi - Maelezo)
Mkurugenzi wa wa EACOM Africa, David Silomba (kulia) akikabidhi  hundi ya thamani ya sh. milioni 10 kwa Mwenyekiti wa  Kituo cha New Hope Family Group Omari  Kombe (kushoto) na katikati ni Kampeni Meneja, Braiton  Balige.

Na Salma Ngwilizi- Maelezo
KITUO cha kulelea watoto waishio mazingira magumu New Hope Family Group kilichopo  kisarawe II-kigamboni, kimewaomba wagombea urais nchini, kuzungumzia suala la kusaidia  watoto yatima  katika ahadi zao.
 
Kauli hiyo  imetolewa leo na Meneja wa kampeni hiyo Bw.Braiton Balige wakati akizungumza na waandishi wa habari leo  jijini Dar es Salaam kuhusu ujenzi wa kituo ambacho kinasaidia jumla ya watoto 154 .
 
“Tumezoea kuwa jukumu la watoto waishio katika mazingira magumu ni la Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Wizara ya Maendeleo ya Jamii, jinsia na Watoto, NGO’s, Taasisi za kidini na watu binafsi pekee,lakini kuna kundi muhimu sana halijahusishwa kundi hilo kama lingehusishwa tungeweza kutatua kabisa matatizo ya watoto waishio katika mazingira magumu,kundi hili ni la wanasiasa.’’alisema Braiton.
 
 Aliongeza kuwa wameanzisha kapu maalum kwa watangaza nia  katika nafasi  ya urais kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho, ambacho kitasaidia kukuza vipaji vyao na kisha kuwawezesha kunza miasha.
 
Katika kusindikiza kampeni hiyo Bw. David Silomba Mkurugenzi BEACOM AFRICA alichangia kwa kutoa hundi yenye thamani ya  kiasi  cha shilingi milioni 10.
 
Katika kufanikisha kukusanya michango hiyo kamati maalumu itakuwepo viwanja vya leaders club kinondoni Juni 20 na 21mwaka huu  kwa ajili ya kupokea michango kutoka kwa wadau mbalimbali wanaowaunga mkono wagombea.

No comments:

Post a Comment