TANGAZO


Wednesday, May 6, 2015

Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho watenga sh. bilioni 6 kujenga viwanda vya kubangua korosho

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania, Mundhir Mundhir akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa viwanda vitatu vya korosho katika Wilaya za Mtwara, Tunduru na Mkuranga kati ya Mfuko Mfuko wa kuendeleza Zao la Korosho Nchini na wataalamu washauri wa kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi cha Jijni Dar es Salaam na Shule ya Elimu ya Biashara katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Mfuko huo Bw. Suleiman Lenga. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa kuendeleza Zao la Korosho Nchini Bw. Athuman Nkinde akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jumatano (Mei 6, 2015) Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa viwanda vitatu vya korosho katika Wilaya za Mtwara, Tunduru na Mkuranga kati ya Mfuko huo na  wataalamu washauri wa kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi cha Jijni Dar es Salaam na Shule ya Elimu ya Biashara katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam . Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bw. Mundhir Mundhir na Katibu Mtendaji wa mfuko huo Bw. Suleiman Lenga 
Mwadili wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Shule ya Elimu ya Biashara, Dkt. Ulingeta Mbamba (kushoto) na Katibu Mtendaji wa Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho Nchini, Bw. Suleiman Lenga wakionyesha mkataba wa ujenzi wa viwanda vitatu vya korosho katika Wilaya za Mtwara, Tunduru na Mkuranga. Hafla hiyo ilifanyika leo Jumatano (Mei 6, 2015) Jijini Dar es Salaam.
1.    Makamu Mkuu wa Chuo cha Ardhi cha Jijini Dar es Salaam, Prof. Gabriel Kassenga (kulia) na Katibu Mtendaji wa Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho Nchini, Bw. Suleiman Lenga wakionyesha mkataba wa ujenzi wa viwanda vitatu vya korosho katika Wilaya za Mtwara, Tunduru na Mkuranga. Hafla hiyo ilifanyika leo Jumatano (Mei 6, 2015) Jijini Dar es Salaam.

Na Ismail Ngayonga, Maelezo
Dar es Salaam
06. Mei, 2015
MFUKO wa kuendeleza zao la Korosho nchini umetenga kiasi cha Tsh Bilioni 6 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vitatu vya kubangulia korosho vitakavyojengwa katika Wilaya za Mtwara, Tunduru na Mkuranga.

Taasisi zitakazojenga viwanda hivyo ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Kitivo cha Biashara na Chuo Kikuu  cha Ardhi (ARU).
Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mikataba baina ya mfuko huo na wataalamu washauri, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, Athuman Nkinde katika bajeti iliyopo kiwanda kimetengewa kiasi cha Tsh Bilioni 2 na pia fedha hizo zinatarajia kuongezeka kila mwaka kulingana na mahitaji yatakavyojitokeza.

Nkinde alisema ujenzi wa viwanda hivyo unatarajia kuanza katika kipindi cha miezi  mitatu ijayo ambapo pindi vitakapomalika kila kiwanda kinataraji kuzalisha tani 10000 kwa mwaka, na kuongeza kuwa Ofisi yake ina imani kubwa ujenzi wa viwanda hivyo utasaidia kuleta mageuzi makubwa ya zao la koroho nchini.

Aliongeza kuwa madhumuni ya kuanzisha viwanda hivyo ni kuliongezea thamani kwa  zao la korosho ili  liweze kuchangia kikamilifu katika kukuza uchumi wa nchi pamoja na wakulima wa zao hilo nchini.

Kwa mujibu wa Nkinde alisema taasisi zilizopewa kazi ya ujenzi wa viwanda hivyo  havina budi kutambua ukubwa wa kazi kwani zipo taasisi nyingi zabuni wa ujenzi huo, hivyo ni wajibu wao kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika kupitia mradi huo.
“Tumeingia katika historia mpya leo hii, dunia nzima itasikia taarifa hizi za ujenzi wa viwanda hivi, hivyo ni wajibu wenu kufanya kazi kwa kuzingatia uwezo wa kitaaluma mliokuwa nao” alisema Nkinde.

“Tanzania imekuwa ikisafirisha nje ya nchi korosho ghafi, kwa kujenga viwanda hivi kutatusaidia kupunguza gharama hizo sambamba na kuongeza thamani ya zao hilo”

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Mfuko huo, Suleiman Lenga aliwataka wataalamuwashauri hao kuzingatia viwango, ubora na muda katika kutekeleza ujenzi wa miradi hiyo kwani  taasisi hizo zina uzoefu mkubwa katika kusimamia na kundeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.
Alisema katika mikataba iliyosainiwa, Chuo cha Ardhi  kitahusika zaidi katika kuandaa michoro, ramani na usanifu wa majengo wakati, Chuo cha Biashara kitahusika katika kuandaa andiko la mradi litakalohusiana na masuala mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa masoko.

Naye Mwadili wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Kitivo cha Elimu ya Biashara, Dkt. Ulingeta Mbamba alisema taasisi itafanya kazi kwa weledi mkubwa ili kuhakikisha kuwa ujenzi huo utafikia katika ubora na viwango vilivyokusudiwa.

“Zao la korosho limekuwa kwa sasa limekuwa ni zao muhimu kwa uchumi wa Tanzania na wananchi kwa ujumla, hivyo tutahakikisha kuwa kupitias ujenzi huu zao hili linazidi kuopngezewa thamani yake” alisema Dkt. Mbamba.


Aidha Makamu Mkuu wa Taaluma katika Chuo Kikuu cha Ardhi, Prof. Gabriel Kassenga  alisema wa Chuo kitahakikisha kuwa viwanda hivyo vitaleta tija iliyokuwa kwa kukuza uchumi wa Taifa na wakulima wa zao la koerosho nchini.

No comments:

Post a Comment