TANGAZO


Friday, January 9, 2015

Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA) wafanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji Ruvu Juu

Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) Didas Mwilawi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha akisalimiana na Mwenyekiti wa wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA Christine Kilindu alipowasili leo, eneo zinapojengwa Ofisi za mradi wa bomba kuu la maji kutoka Ruvu Juu zilizopo Kibaha. (Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO)
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) wakiwa wameanza ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) wakiwa ndani ya tangi la maji eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakijionea ukarabati unaoendelea ili kuboresha upatikanaji wa maji jijini.
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wakiangalia maungio ya mradi wa bomba jipya kutoka mtambo wa Ruvu Chini yaliyopo eneo la Mpiji wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani. 
Sehemu ya maungio ya mradi wa bomba jipya kutoka mtambo wa Ruvu Chini yaliyopo eneo la Mpiji wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) kukagua mabomba yaliyohifadhiwa eneo la Kibaha Mwendapole wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
 Meneja wa Mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu Pintu Dutta kwa kampuni ya VA TECH WABAG kutoka India akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) walipotembelea huo eneo la upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
Meneja wa Mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu Pintu Dutta kwa kampuni ya VA TECH WABAG kutoka India akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) walipotembelea huo eneo la upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wakitembelea sehemu unapofanyika upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wakiangalia moja ya matangi ya maji sehemu unapofanyika upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu.
 Msingi wa moja kati ya matangi matatu yanayojengwa yakiwa ni upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu.
 Mafundi wakiendelea na shughuli ya upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu.
Sehemu ya mtambo wa Ruvu Juu kabla ya upanuzi. 
Moja ya hatua ya kusafisha maji katika mtambo wa Ruvu Juu kabla ya kusafirishwa tayari kwa matumizi kwa wakazi wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. 


Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
WAJUMBE wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wamefanya ziara ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.

Ziara ya wajumbe hao wa kamati Ufundi ilianza kwa kukagua kazi ya ukarabati wa kituo yalipo matangi ya maji eneo la Chuo Kiukuu cha Dar es salaam, maungio ya mradi wa bomba jipya yaliyopo eneo la Mpiji, ujenzi wa ofisi ya mradi wa bomba kuu la maji kutoka Ruvu Juu zilizopo Kibaha, kukagua mabomba yaliyohifadhiwa eneo la Kibaha Mwendapole na upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu Mladizi na Ruvu darajani.  

Akifanya majumuisho ya ziara hiyo Mwenyekiti wa wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA Christine Kilindu amesema kuwa wajumbe wameridhishwa na kasi ya ujenzi wa miundo mbimu hiyo ambapo matarajio mradi huo utakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa mwishoni mwa mwaka huu.

Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa wananchi wa mikoa ya Dar es salaam na Pwani watarajie kupata huduma ya maji iliyo bora mara miradi ya Ruvu Juu Chini itakapokamilika.

Aidha, Christine amewaasa wananchi wa maeneo yanapopita mabomba wa miradi hiyo kuyatunza vizuri kuanzia wakati huu yalipohifadhiwa na yatakapokuwa yameanza kutumika ili yawanufaishe wananchi wote wa mikoa hiyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi DAWASA Romanus Mwang’ingo alisema kuwa pamoja na kuboresha huduma kwa maeneo yaliyo pembezoni mwa barabara ya Morogoro yaani Kimara, Mbezi, Kiluvya, Kibaha, Visiga, Mlandizi na Kibamba, utekelezaji huo pia utawanufaisha wakazi wa Ubungo, Vingunguti, Kimara, Tabata na Kinyerezi ambao nao wanahudumiwa na mtambo unaotoa maji kutoka Ruvu Juu.

Mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Chini unalenga kuongeza uzalishaji maji na kuwahudumia wakazi wa maeneo ya uwekezaji (EPZ), Chasimba, Buma, Zinga, Kerege, Mpiji, Bunju, Wazo, Salasala, Madale, Kinzudi, Mbezi Juu, Goba, Kawe, Makongo, Mwenge, Msasani, Mikocheni, Mlalakua, Masaki, Sinza, kijitonyama, Manzese, Konondoni, Magomeni, Kigogo, Vingunguti, Buguruni, Kariakoo na Ilala.


Kazi hiyo ya maboresho inafanyika chini ya mpango maalumu wa kuboresha huduma ya upatikanaji wa Maji Safi na Maji Taka jijini Dar es salaam na maeneo mengine yanayohudumiwa na DAWASA unaohususha ujenzi wa miradi mipya na pamoja na kukarabati miundombinu iliyopo. 

No comments:

Post a Comment