TANGAZO


Saturday, November 29, 2014

Tandika Vicoba Group yazinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Margareth Chacha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Margareth Chacha (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tandika Vicoba Group (Tavico), uliofanyika katika viwanja vya Kanisa Katoliki la Chang'ombe Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tavico, Sarah Chikuni, wengine ni wanachama.
Keki maalumu ya sherehe hiyo ilivyokuwa ikionekana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Margareth Chacha (kulia), pamoja na Mwenyekiti wa Tavico, Sarah Chikuni wakikata keki maalumu ya uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya Kanisa Katoliki la Chang'ombe Dar es Salaam jana.
Hapa ni mserebuko kwa kwenda mbele.
Wanachama wa Tandika Vicoba Group (Tavico), pamoja na wageni waalikwa wakiserebuka katika hafla ya uzinduzi wa Tavico uliofanyika viwanja vya Kanisa Katoliki la Chang'ombe Dar es Salaam.


Wanachama wa Tavico wakiwa kwenye hafla hiyo.
Wanachama wa vicoba kutoka Yombo Makangarawe nao walijumuika katika uzinduzi huo.
Hapa wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Maofisa kutoka Tavico, Mariam Shabani (kushoto) na Mariam Ndunguru ambaye ni mlezi wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Tavico, Sara Chikuni akimkaribisha mgeni rasmi, Mama Chacha katika sherehe hiyo.


Ni furaha tupu katika uzinduzi huo.


Ni kuserebuka tu. Chezea uzinduzi wewe mbona raha.
Maofisa wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), nao walikuwepo. Kutoka kushoto ni Masanyika Choka na Sunday Mziray.
Wanahabari nao walikuwepo kuchukua taarifa hiyo.
Tuserebuke tuserebuke mpaka chini. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com)

No comments:

Post a Comment