Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (katikati)akiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Meja Mstaafu Juma Kassim Tindwa wakifuatilia kwa makini Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alipokuwa akiwwapisha Manaibu Katibu Wakuu Wizara mbali mbali za Serikali na Wakuu wa Wilaya mbali mbali za Unguja na Pemba katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Mwanasheria Mkuu wa Serkali ya Mapinduzi ya Zanzibar Said Hassan Said (kulia) akiwa na Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali ni miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika Viapo mbali mbali vya Wakuu wa Wilaya za Zanzibar na Katibu Mkuu na Manaibu Katibu wakuu wa Serikali waliapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
Mawaziri waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Wakuu wa Wilaya mbali mbali za Unguja na Pemba pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Wizara mbali mbali za Serikali wakifuatilia kwa makini walipokuwa wakiapishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Khamis Jabir Makame kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo kabla alikuwa Mkuu wa Wilaya Kaskazini B Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Haji Makungu Mgongo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Unguja katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo kabla alikuwa Mkuu wa Wilaya Kusini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Hassan Khatib Hassan kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete Pemba katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bibi Khadija Bakari Juma kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Bi Madina Mjaka Mwinyi kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Dkt. Said Seif Mzee kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Dkt. Juma Yakout Juma kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi mbali mbali katika
hafla iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
katika hafla hiyo ni Bwana Khamis Jabir Makame ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya
Kusini Unguja ambapo kabla ya uteuzi wake huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya
Kaskazini ‘B’ Unguja, Luteni Kanali
Mstaafu Haji Makungu Mgongo ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’
Unguja ambapo kabla ya hapo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja.
Bwana Hassan
Khatib Hassan ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete, Bibi Khadija Bakari Juma
ambaye ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Bibi
Madina Mjaka Mwinyi ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Amali.
Wengine ni Dk.
Said Seif Mzee ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara, Viwanda na
Masoko, Dk. Juma Yakout Juma, ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa
na viongozi mbali mbali wakiwemo baadhi
ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Mhe. Said Hassan Said, Mkuu wa Mkoa wa
Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja
Meja Mstaafu Kasim Tindwa, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali pamoja na Washauri wa Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali.
No comments:
Post a Comment