*Matokeo ya
ufaulu sasa hayatabadilika
*Watakaofanya
vibaya hawana pa kuponea
Na Mwandishi wetu
BARAZA la Mitihani la Tanzania(NECT), limetangaza mfumo mpya wa upangaji ufaulu kwa mitihani ya
kidato cha nne na cha sita ambao sasa watatumia mfumo wa wastani wa pointi.
Kwa mujibu wa baraza hilo ni kwamba mfumo huo wa wastani wa
pointi hautakuwa wa kubadilika ambao ni tofauti na ule uliokuwa unatumjiwa
awali ambapo viwango vya ufaulu vinaweza kubadilika.
Akitangaza mfumo huo Dar es Salaam leo, Katibu Mtendaji wa
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde alisema katika mfumo
wa viwango vya ufaulu visivyobadilika ,viwango vya ufaulu vinavyofanana
hupangwa ili viwe kipimo cha ufaulu kwa masomo yote kila mwaka.
“Kuanzia mwaka 1973 hadi mwaka 2011 Baraza la Mitihani
lilikuwa likitumia mfumo wa viwango vya ufaulu vinavyobadilika.
“Hata hivyo kwa kuzingatia maoni ya wadau wa elimu kuanzia
mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012 ,baraza liliamua kutumia mfumo wa viwango
vya ufaulu visivyobadilika,”alisema Dk.Msonde.
Alifafanua ili kupata viwango vya ufaulu visivyobadilika
,baraza lilizingatia wastani wa viwango vya ufaulu vilivyotumika kuanzia mwaka
1999 hadi mwaka 2011.
Alisema baraza lililenga kupunguza mlundikano wa alama na kuwianisha viwango vya alama za mitihani ya
kidato cha nne (CSEE) na mtihani wa kidato cha Sita (ACSEE).
Pamoja na hayo alisema ipo mifumo anuwai inayotumiwa na nchi
mbalimbali duniani katika kupanga viwango vya ufaulu vinavyobadilika na mfumo
wa viwango visivyobadilika.
Alisema katika mfumo wa viwango vinavyobadilika ,viwango vya
ufaulu hupangwa kwa kutegemea jinsi watahiniwa walivyofaulu somo husika.
Katika
mfumo wa ufaulu usiobadilika , viwango vya ufaulu vinavyofanana hupangwa ili
viwe kipimo cha ufaulu kwa masomo yote kila mwaka.
Dk.Msonde alifafanua mifumo inayotumika kupanga madaraja ya
ufaulu ni mfumo wa jumla ya pointi na mfumo wa wastani wa pointi.
Alisema mfumo wa jumla ya pointi ni mfumo ambao madaraja ya
ufaulu hupangwa kwa kutumia jumla ya pointi .Mfumo huo umekuwa ukitumika
kuanzia mwaka 1973 hadi mwaka 2014 kulingana na muongozo wa matumizi ya viwango
vya ufaulu na utaratibu wa kutunuku matokeo ya mtihani wa kidato cha nne na cha
sita uliotolewa mwaka 2014,uzito wa alama
katika gredi A (1), B+ (2), B (3),
C (4), D (5), E (6) na F (7).
“Katika mfumo wa jumla ya pointi , madaraja ua ufaulu
hupangwa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne.Daraja I-III hubainishwa kwa
idadi ya pointi alizopata mtahiniwa wakati daraja la Nne hubainishwa kwa
kutumia kigezo cha mtahiniwa kafaulu angalu D mbili au C moja ama zaidi.
“Daraja la ufaulu wa mtihaniwa , kwa kidatoi cha nne hupangwa
baada ya kupata jumla ya pointi alizopata katika masomo saba aliyofanya vizuri.
“Kwa mtahiniwa wa kidato cha Sita, daraja hupangwa baada ya
kupata jumla ya pointi azilizopata katika masomo matatu ya
tahasusi(Combination)
Kuhusu faida za mfumo mpya , alisema baraza linaona kuwa
kutumia mfumo wa wastani wa pointi utawezesha kuwa na mfumo wa kutunuku matokeo
wa aina moja katika ngazi zote za mafunzo kuanzia elimu ya msingi hadi elimu ya
juu, matokeo yaliyo katika mfumo wa wastani wa pointi kwenye cheti
yatarahisisha kazi ya udahili wa watahiniwa unaofanywa na TCU na NACTE katika ngazi za juu za mafunzo.
Pia mfumo wa wastani wa pointi ni rahisi kueleweka kwa wadau
wa kada mbalimbali kwasababu hutoa tafsiri yenye kuonesha mtahiniwa aliye na
GPA kubwa ndiye aliye na matokeo mazuri.
Pamoja na hayo, alisema baraza limeona ni vema likaendelea
kutoa elimu kwa wadau kuhusu mfumo wa kutunuku matokeo ya mtihani wa kidato cha
Nne na cha Sita.Nia ya baraza ni kuhakikisha wadau wanakuwa na taarifa sahihi
na uelewa wa namna mfumo huo unavyotumika.
No comments:
Post a Comment