TANGAZO


Saturday, August 30, 2014

Mwandishi ajitosa uchaguzi wa Chadema


Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zanzibar, Bi. Maryam Ahmed Omar, akimkabidhi mwanachama Salum Mwalim, fomu ya kugombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, kundi la Zanzibar katika hafla fupi iliyofanyika Ofisi Kuu ya Chadema kisiwani humo leo. (Picha zote na Martin Kabemba)


Mmoja wa wachama wa Chadema Zanzibar, Bikwao Khamis akitia saini fomu ya udhamini wa Salum Mwalim (aliyesimama, wa kwanza kushoto) anaegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, kundi la Zanzibar. Mwalim amechukua na kurudisha fomu hiyo leo, Jumamosi, Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar.

Mwenyekiti wa Chadema, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, Jumbe Idrisa akitia saini fomu ya udhamini wa mwanachama Salum Mwalim (aliyesimama, wakwanza kushoto) anayegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, kundi la Zanzibar. Mwalim amechukua na kurudisha fomu hiyo, leo Jumamosi, Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar.

Mbunge wa Chadema, viti maalum, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mwanamrisho Abama akimdhamini Mgombea Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Salum Mwalim katika Ofisi za chama hicho, Zanzaibar. Mwalim amechukua na kurudisha fomu hiyo leo, Jumamosi, Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema, mjini Zanzibar.
Salum Mwalim anayewania nafasi ya ujumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, kundi la Zanzibar, akitiasaini kitambu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi Kuu za chama hicho, mjini Zanzibar leo, kwa lengo la kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment