TANGAZO


Friday, February 21, 2014

Ukraine:Hatimaye makubaliano yapatikana

Katibu mkuu wa UN Ban Ki Moon amesema kuwa hali Ukraine ni ya kutamausha
Habari za hivi punde zinaarifu kuwa ofisi ya rais Yanukovych nchini Ukrain imetoa taarifa inayosema kwamba mwafaka umefikiwa katika mazungumzo ya usiku kucha kati ya serikali, upinzani na waakilishi wa Muungano wa Ulaya na Urusi.
Taarifa hiyo hata hivyo haikutoa maelezo zaidi kuhusu makubaliano hayo ingawa ilisema kuwa pande zote zitatia saini makubaliano yenyewe.
Duru zinasema kuwa Rais Yanukovych amekuwa akikabiliwa na shinikizo apange uchaguzi wa mapema pamoja na mageuzi ya kikatiba.
Umoja wa Ulaya umekubali kuwawekea vikwazo viongozi waliopanga ghasia zinazoikabili Ukraine kwa sasa.
Uamuzi huo uliofanyika mjini Brussels, Ubelgiji umejiri baada ya watu kadhaa kuuawa mjini Kiev, katika siku ambayo ilishuhudia umwagikaji mkubwa zaidi wa damu tangu uhuru wa Ukraine zaidi ya miaka ishirini iliyopita.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Italia, Emma Bonino, amesema vikwazo hivyo vinavyojumuisha vya usafiri na kupiga tanji mali za wahusika na kwamba vinawalenga wale waliohusika na mauaji ya waandamanaji.
Ujumbe wa Umoja wa Ulaya mjini Kiev unajaribu kuwapatanisha viongozi wa upinzani na rais Victor Yanukovych ili kuleta amani na pia kushawishi taifa hilo kuandaa mapema uchaguzi uliopangiwa kufanyika mwaka ujao.
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa, Ban Ki-moon amesema hali nchini Ukraine ni ya kutamausha:
Wito huo umetolewa vile vile na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry ambaye ametaka vurugu kusitishwa nchini Ukraine akisema kuwa watu wa taifa hilo wanastahili kuwa na hali bora kuliko kile alichokitaja kuwa maafa na mateso yasiyofaa ambayo yameshuhudiwa katika barabara za mji mkuu, Kiev.
Haijabainika ni watu wangapi waliouwawa katika vurugu za Alhamisi lakini wizara ya Afya inasema tangu Jumanne, watu sabini wameuawa na zaidi ya 570 wamejeruhiwa.

No comments:

Post a Comment