TANGAZO


Saturday, February 15, 2014

Ndoa za jinsia moja zapingwa Uingereza



Wanandoa wa jinsia moja
Maskofu wakuu katika kanisa moja nchini Uingereza wamewaambia viongozi wa dini kwamba hawataruhusiwa kuingia katika ndoa za jinsia moja,na kusema kuwa hawatakubali viongozi wa dini masenge kwenda kinyume na maagizo hayo.
Viongozi wa dini wa kanisa la Ki-Anglikana wanakubaliwa na kanisa hilo kuingia katika uhusiano wa kimapenzi lakini kwa maelewano kwamba hawatashiriki ngono.
Katika mwelekeo wao, maaskofu hao pia wamepiga marufuku maombi yoyote maalum kwa wanadoa wa jinsia moja licha ya ripoti rasmi ya kanisa hilo kupendekeza kwamba viongozi wa dini wanaweza kufanya hivyo iwapo wanajihisi.
Hatahivyo amesema kuwa viongozi wa dini wanapaswa kutoa maombi yasio rasmi kwa wanandoa walio katika uhusiano wa jinsia moja.

No comments:

Post a Comment