TANGAZO


Wednesday, January 8, 2014

Puntland yapata Rais Mpya

 

Wabunge wa Puntland ndio humchagua Rais
Wabunge katika jimbo la Puntland nchini Somalia wamemchagua waziri mkuu wa zamani wa Somalia Abdiweli Muhammad
kama Rais mpya wa jimbo hilo linalojitawala ingawa linasema liko chini ya Somalia.
 
Abdiweli, alimshinda Rais Abdirahman Muhammad Farole kwa kura 33 kwa 32 katika duru ya tatu na ya mwisho kutokana na wagombea kukosa kupata zaidi ya thuluthi moja ya kura zilizohitajika kuibuka mshindi.
 
Hali ya usalama ilidhibitiwa vikali wakati wa uchaguzi huo ambapo ni wabunge waliomchagua Rais mpya.

Wagombea 11 waligombea katika duru ya kwanza lakini ni wagombea watatu pekee waliofanikiwa kupata idadi kubwa ya kura na kwenda katika awamu ya pili na ya tatu.

Farole alifanikiwa kupata kura 27 kati ya kura 66 katika awamu ya kwanza ya uchaguzi wenyewe huku Ali akipata kura 13.

Katika awamu ya pili,Farole alipata kura 31, Ali akapata 18 huku mgombea wa tatu Warsame akipata kura 16. Warsame, kutokana na kupata kura chache zaidi katika awamu ya pili hakuweza kufanikiwa kwenda katika raundi ya tatu.

Hii ni mara ya tatu kwa Puntland kufanya uchaguzi kama huu tangu kujitenga na Somalia mwaka 1998.

Bunge la jimbo hilo lina wabunge 66 waliochaguliwa na wazee wa kikoo mwaka 2013.

Ali, alikuwa waziri mkuu wa Somalia kati ya Juni mwaka 2011 na Oktoba mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment