TANGAZO


Thursday, January 2, 2014

Hali ya Ariel Sharon yazorota zaidi

 


Sharon alisifika zaidi kwa msimamo wake mkali wa kisiasa

Hali ya kiafya ya waziri mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon - ambaye amekuwa katika hali mahututi, inaendelea kuzorota zaidi.
Inaarifiwa kwamba maisha yake yamo hatarini.
 
Madaktari wanasema kuwa Sharon mwenye umri wa miaka , 85, anakabiliwa na matatizo ya afya ya viongo vyake vya mwili ikiwemo Figo zake na kwamba vinaanza kuonekana kutofanya kazi vyema.
Hata hivyo madaktari hawakutoa taarifa zaidi kuhusu afya ya Sharon.
Alichukua wadhifa wa waziri mkuu mwaka 2001 na kuugua kiharusi mwaka 2005 na alisifika sana kwa msimamo wake mkali kuhusu hali ya kisiasa kati ya taifa hilo na utawala wa Palestina.
Baada ya kupatwa na kiharusi kingine mwaka 2006, Sharon akapotewa na fahamu na amekuwa kwenye mashine ya kusaidia moyo wake kuendelea kupiga tangu hapo.
Sharon alikuwa mmoja wa wanasiasa mashuhuri wenye utata katika siasa za Israel.

No comments:

Post a Comment