TANGAZO


Saturday, November 16, 2013

Mapambano yaendelea mitaani Tripoli

 

Majuruhi katika maandamano ya Tripoli
Ripoti kutoka mji mkuu wa Libya, Tripoli, zinaeleza kuwa mapambano mengine yametokea siku moja baada ya watu wengi kuuwawa na kujeruhiwa kwenye maandamano ya kupinga makundi ya wanamgambo.
Ghasia zinatokea katika mitaa ya mashariki mwa Tripoli baina ya wanamgambo wa mji na wapiganaji kutoka mji wa Misrata.
Katika ghasia za Ijumaa wanamgambo wa Misrata walifyatua risasi dhidi ya waandamanaji waliodai kuwa wanamgambo hao waondoke Tripoli.
Wizara ya Afya inasema watu 43 waliuwawa Ijumaa na 500 kujeruhiwa kwenye ghasia hizo, ambapo waandamanaji nao walijibiza shambulio dhidi ya wanamgambo.
Waziri Mkuu, Ali Zeidan, ameziomba pande zote mbili kuwa na ustahmilivu.

No comments:

Post a Comment