Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete akitoa hotuba wakati wa kuweka jiwe la msingi la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha mkoani Pwani. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete (wa kwnza kulia), akiteta jambo na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda (katikati) na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi, wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani. Balozi wa Cuba nchini, Jorge Luis Lopez Tarmo (wa kwanza kulia), akimkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete, zawadi ya picha ya hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere na Fidel Castro wakati hafla ya kuweka jiwe la msingi la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa LABIOFAM, Dk. Jose Frag Castro akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Dk. Chrisant Mzindakaya (kulia), wakati akiwasili katika viwanja vya eneo la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani.Baaadhi ya wafanya kazi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), wafanyakazi wa LABIOFAM na wageni waalikwa wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani), Rais Kikwete, wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani. Picha ya pamoja ya Rais, Dk. Jakaya Kikwete na wageni waalikwa mara baada ya kuweka jiwe la msingi la kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani. Rais Dk. Jakaya Kikwete, akitembelea baadhi ya sehemu za Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria, mara baada ya kuweka jiwe la msingi la Kiwanda hicho leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha mkoani Pwani. Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akisalimiana na akina mama, mara baada ya kuwasili katika viwanja vya eneo la Kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wa malaria leo, kilichopo nje kidogo ya mji wa Kibaha, mkoani Pwani.(Picha zote na Eleuteri Mangi-Maelezo)
No comments:
Post a Comment