TANGAZO


Tuesday, October 1, 2013

Michezo ya SHIMIWI, Utumishi yaingia Robo Fainali

Timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma kabla ya kuanza kwa mechi kati yake na timu ya Wizara ya Katiba na Sheria katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria  kabla ya kuanza kwa mechi kati yake na timu ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma. 
Timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma kabla ya kuanza kwa mechi kati yake na timu ya Wizara ya Katiba na Sheria katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Timu ya mpira wa pete ya Utumishi ikisalimiana na timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria kabla ya mpambano katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Mchezaji wa timu ya mpira wa pete ya Utumishi Amina Ahmed (WD) akijaribu kutoa pasi wakati timu yake na timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria zilipokutana katika mashindano ya SHIMIWI Dodoma.
Timu ya mpira wa pete ya Utumishi ikimenyana na timu ya mpira wa pete ya  Wizara ya Katiba na Sheria zilipokutana katika mashindano ya SHIMIWI mjini Dodoma.
 Mchezaji wa timu ya mpira wa pete ya Utumishi Perice Makau (GS) akijaribu kufunga wakati wa mpambano kati ya timu ya mpira wa pete ya Utumishi na timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria katika mashindano ya SHIMIWI mjini Dodoma.
Mchezaji wa timu ya mpira wa pete ya Utumishi Perice Makau (GS) akijaribu kutoa pasi wakati wa mpambano kati ya timu ya Utumishi na timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria katika mashindano ya SHIMIWI mjini Dodoma.Utumishi ilishinda kwa mabao 40-8.
Mchezaji wa timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria Joyce Nkoliala (aliyelala chini) akipewa huduma ya kwanza baada ya kuanguka uwanjani wakati wa mechi kati ya timu 
ya mpira wa pete ya Utumishi na timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Katiba na Sheria mjini Dodoma.

Na Happiness Shayo
Timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma imefanikiwa kuingia katika robo fainali ya mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayoendelea mjini Dodoma baada ya kuifunga timu ya Wizara ya Katiba na Sheria mabao 40-8 jana katika viwanja vya Jamhuri.

Katika mchezo huo,Utumishi iliendelea kufanya vizuri kwa kuwatumia wafungaji wake Perice Makau (GS) aliyefunga mabao 16 na Anna Msulwa (GA) aliyefunga mabao 4 na kuipatia timu hiyo mabao 20 katika kipindi cha kwanza huku timu ya Wizara ya Katiba na Sheria ikifunga mabao 5 kupitia wafungaji wake Hidaya Hoza (GA) aliyefunga mabao 4 na Rukia Mlingi (GS) aliyefunga bao 1.

Kipindi cha pili cha mchezo, mpira ulionekana kuelemea timu ya Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kufungwa mabao 20-3 na timu ya Utumishi.

Akiongea mara baada ya mechi hiyo,kocha wa timu ya Utumishi Bw.Mathew Kambona alisema kuwa pamoja na kufanya vizuri katika mechi hiyo lakini alitumia wachezaji wa kawaida na kupumzisha wachezaji mahiri kwa ajili ya mechi ya robo fainali.

“Mchezo wa leo ni mzuri lakini nimeamua kutumia wachezaji wa kawaida ili kujiandaa na mchezo wa robo fainali kati yetu na TAMISEMI utakaochezwa jumatano ya wiki hii katika viwanja vya Jamhuri”alisema Bw.Kambona.

Pia,Bw.Kambona alisema kuwa timu ya Utumishi imejipanga vizuri ili kuhakikisha inaendelea na moto huohuo wa kutoa vichapo kwa wapinzani wake hadi kufikia fainali za mashindano hayo.
Naye kocha wa timu ya Katiba na Sheria Bw.Paulo Mathias alisema kuwa timu yake imekubali matokeo kwa kuwa imezidiwa na timu ya Utumishi.

“Kufungwa ni kitu kinachotokea ndani ya uwanja kwa hiyo sina budi kukubali matokeo kuwa timu yangu imezidiwa uwezo na timu ya Utumishi”alisema Bw.Mathias.

Mashindano ya SHIMIWI yako katika mtoano wa kuingia robo fainali ambapo washindi watafanikiwa kuingia nusu fainali.Michezo inayochezwa ni mpira wa miguu,mpira wa pete,karata,kurusha tufe,riadha na kucheza bao.

No comments:

Post a Comment