TANGAZO


Sunday, October 6, 2013

Japan yasaini mkataba wa kuisaidia Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Wama Nakayama inayosimamiwa na Mama Kikwete


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kulia), akimpokea Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada (katikati). Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya watoto yatima, wanaoishi katika mazingira hatarishi (Wama Nakayama), Ramadhani Dau, wakati alipotembelea shule hiyo jana, iliyopo Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. 
Rais Jakaya Kikwete (kulia), akisalimiana na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada,  wakati  walipotembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana yatima, wanaoishi katika mazingira hatarishi ya Wama Nakayama, Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani jana. Katikati ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dk. Ramadhani Dau.

Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, akizungumza jambo na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada (kushoto) na  Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dk. Ramadhani Dau (katikati), wakati wa ziara hiyo jana. 

Rais Jakaya Kikwete  akisalimiana na Mwalimu wa masomo ya Kiingereza na Uraia wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya watoto yatima, wanaoishi katika mazingira hatarishi (WAMA Nakayama), Sophia Shafii wakati alipotembelea shule hiyo, leo wilayani Rufiji, mkoani Pwani.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete (wa tatu  kushoto) na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada ( wa pili kulia) wakitia saini   mkataba wa msaada wa kutayarisha vifaa vya maabara, ujenzi wa zahanati na kutoa mtambo wa maji wa kutumia jenereta, wenye thamani ya sh. milioni 170 kwenye  Shule ya Sekondari ya Wasichana, yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi (WAMA Nakayama). Kulia wa kwanza ni Rais Jakaya Kikwete na kushoto wa pili ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Ramadhani Dau. Kushoto, wa  kwanza  ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Suma  Mensah. Hafla hiyo fupi, imefanyika jana, katika  shule hiyo,  iliyopo wilayani Rufiji, mkoani Pwani.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, akionesha mkataba aliosaini pamoja na Balozi wa Japan nchini, Masaki  Okad (wa pili kulia), kusaidia vifaa vya maabara, ujenzi wa Zahanati na mtambo wa maji wa kusukumwa na jenereta, wenye thamani ya jumla ya sh. milioni 170 kwa shule hiyo. Kulia ni mumewe, Rais Jakaya Kikwete,  Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Suma  Mensah (kushoto) na Mwenyekiti wa bodi ya shule, Dk. Ramadhani Dau. 
Rais  Jakaya Kiwete (katikati),  akitembelea shule hiyo, iliyopo wilayani Rufiji,  mkoa wa Pwani. Kushoto anayemtembeza ni Mwalimu Mkuu wa shule, Suma  Mensah na kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya shule, Dk. Ramadhani Dau.
Rais Jakaya Kiwete, akisoma moja ya kitabu cha somo la Fizikia katika maktaba ya Shule ya Sekondari ya Wasichana, yatima, wanaoishi katika mazingira hatarishi (WAMA Nakayama) jana, iliyopo wilayani Rufiji mkoa wa Pwani wakati alipotembelea shule hiyo katika ziara yake. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Suma  Mensah.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete (aliyevaa kitenge), akizungumza jambo na Balozi wa Japan nchini, Masaki  Okada (wa pili kushoto), wakati alipokuwa akitembelea  Shule ya  Sekondari ya Wasichana, ya yatima, wanaoishi katika mazingira hatarishi (WAMA Nakayama). Kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Ramadhani Dau.


Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama), Daudi Nasib (katikati), akibadilishana mawazo na Naibu wa Waziri wa Chakula (kulia), Adam Malima na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif  Rashid,    wakati wa hafla hiyo. (Picha zote na Magreth Kinabo, Maelezo)

No comments:

Post a Comment