TANGAZO


Wednesday, May 29, 2013

Rais wa Zanzibar Dk. Shein na Ujumbe wake watembelea mji wa Kihistoria jijini Beijing, ashuhudia utiaji saini makubaliano ya kibiashara kati ya nchi hizo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo wakati alipotembelea sehemu za Kihistoria zilizopo katika mji wa Beijing nchini China kiwa katika ziara ya Kiserikali na ujumbe wake. (Picha na Ramadhan Othman, China)
 Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwamamwema Shein, akiangalia kitabu wakati alipotembelea makumbusho ya kihistoria katika Mji wa Beijing  nchini China, katika ziara ya Kiserikali kwa mwaliko wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Kulia ni Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi zake Zanzibar, Bibi Chen Qiman.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifuatana na ujumbe wake wakitembelea sehemu mbalimbali za  Kihistoria zilizopo katika Makumbusho ya Mji wa  Beijing, nchini China akiwa katika ziara ya Kiserikali.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifuatana na mkewe, Mama Mwamamwema Shein katika Viwanja vya Makumbusho ya Kihistoria nchini China pamoja na ujumbe waliofuatana nao katika ziara ya Kiserikali.
 Pichani linaonekana  moja wapo ya Majengo yaliyokuwemo katika eneo kubwa la kumbukumbu za kihistoria katika mji wa Beijing, ambapo wananchi wa China wamekuwa na ukarimu wa aina yake.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (wa tatu kusoto), pamoja na ujumbe aliofuatana nao, akiuliza swali kwa waongozaji na watoa maelezo katika sehemu za kihistoria zenye kumbukumbu nyingi, zinazotembelewa na wageni mbalimbali  katika mji huo, wa Beinjing nchini China, akiwa katika ziara ya Kiserikali ya siku saba.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akiuliza suala kwa waongozaji na watoa maelezo katika sehemu za kihistoria zenye kumbukumbu nyingi, zinazopelekea wageni wa aina tofauti kutembelea katika mji huo wa Beinjing nchini China.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na Naibu Waziri wa Biashara wa China Liu Cigui, wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa World Hotel China, ambapo walifanya mazungumzo na kutiliana saini makubaliano ya masuala ya Biashara.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi wa Maendeleo, Omar Yussuf Mzee, akitiliana saini makubaliano ya kibishara kwa upande wa Serikali ya Zanzibar na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Liu Cigui katika ukumbi wa mikutano wa China World Hotel, huku wakishudiwa na baadhi ya Mawaziri na Maofisa wa Serikali zote mbili, za Zanzibar na China.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi wa Maendeleo, Omar Yussuf Mzee, akibadilishana hati walizosaini mkataba ya uhusiano wa Biashara na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Liu Cigui, katika ukumbi wa mikutano wa China World Hotel.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akipeana mkono wa shukurani na Naibu Waziri wa Biashara wa China Liu Cigui, baada ya kutiliana saini makubaliano katika nyanja za kibiashara kati ya Serikali ya China na Zanzibar, ukumbi wa mikutano wa World Hotel China. 

No comments:

Post a Comment