TANGAZO


Thursday, April 25, 2013

Warembo wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean watembelea Ofisi za Jambo Leo

Mwandishi mwandamizi wa Gazeti la Jambo Leo, Eben-ezeri Mende (wa pili kushoto), akimtambulisha  Mhariri Mkuu wa Jambo Leo, Anicetus Mwesa, kwa warembo  wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean, wakati walipotembelea gazeti hilo kujionea jinsi linavyotayarishwa, ikiwemo uwekwaji wa habari mbalimbali, Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)
 
 Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Anicetus Mwesa (kushoto), akiwaonesha warembo  wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean, gazeti hili jinsi linavyotayarishwa, ikiwemo uwekwaji wa habari mbalimbali. Wa pili kushoto ni Mwandishi mwandamizi, Eben-ezeri Mende.
 
Mpigapicha Mkuu wa Gazeti hilo, Richard Mwaikenda akiwaelezea warembo hao, jinsi ya upatikanaji wa picha za habari na jinsi ya kuziandikia maelezo yake kabla ya kuwekwa gazetini jana.

Mhariri wa Michezo, Deo Myonga, akiwaonesha warembo hao, habari za michezo na burudani, jinsi zinavyoandikwa na kupangwa kwenye kurasa za gazeti, walipotembelea Ofisi za gazeti la chumba cha habari jijini leo.

Mhariri wa habari wa Jambo Leo, Julian Msaki (wa kwanza kulia), akiwapatia maelezo warembo hao, kuhusu ukusanyaji wa habri za gazeti za kila siku. Wa pili kulia ni Mwandishi mwandamizi wa Gazeti la Jambo Leo, Eben-ezeri Mende.

Msanifu kurasa wa Jambo Leo, Chris Shola, akiwaonesha warembo hao, jinsi gazeti hilo, linavyosanifiwa.

Mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Jambo Concepts, inayomiliki magazeti ya Jambo Leo, Staa Spot, Dar Metro na jarida la Jambo Brand, Beny Kisaka (kulia), akizungumza na warembo wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean, wakati walipomtembelea ofisini kwake pamoja na kutembelea chumba cha Habari cha magazeti hao, Dar es Salaam leo.

Mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Jambo Concepts, inayomiliki magazeti ya Jambo Leo, Staa Spot, Dar Metro na jarida la Jambo Brand, Beny Kisaka (kulia), akizungumza jambo na warembo hao, walipomtembelea ofisini kwake leo.

Warembo wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean, wakiwa katika picha mara baada ya kumaliza ziara yao, Ofisi za Gazeti la Jambo Leo, Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment