TANGAZO


Friday, April 5, 2013

Makamu wa Rais, Dk. Bilal ashiriki shughuli za kuuaga mwili wa marehemu Jaji mstaafu, Ernest Mwipopo



Majaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, 
Justice Ernest Mwipopo, wakilishusha katika gari kwa ajili ya 
kuanza shughuli za kuaga katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo. (Picha zote na OMR)



Majaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, 
Justice Ernest Mwipopo, wakilishusha katika gari kwa ajili ya 
kuanza shughuli za kuaga katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo.



Mmoja wa Majaji, akibeba picha ya marehemu Justice Mwipopo, 

wakati majaji hao, wapokuwa wakilishusha jeneza, lenye mwili wa 

marehemu huyo, kwa ajili ya kuanza shughuli za kuuaga, Viwanja 

vya Karimjee leo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Jaji Mkuu Kiongozi, Fakhi Jundu (kushoto) na Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othmani, wakati akiwasili kwenye Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo, kushiriki kwenye shughuli za kuuaga mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa ajali ya gari, April 3, huko maeneo ya Morogoro.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Jaji mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa ajali ya gari April 3, huko maeneo ya Morogoro. Shughuli hizo za kuaga mwili huo, zimefanyika leo, April 5, 2013, Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya shughuli hizo, mwili huo, ulisafirishwa kuelekea mkoani Iringa kwa maziko kesho. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia, Dk.

Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji ndugu wa marehemu baada ya 

kutoa heshima za mwisho, wakati wa shughuli za kuuaga mwili wa 

marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa 

ajali ya gari April 3, huko maeneo ya Morogoro. Shughuli hizo za 

kuuaga mwili huo, zimefanyika leo April 5, 2013, Viwanja 

vya Karimjee jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya shughuli hizo 

mwili ulisafirishwa kuelekea mkoani Iringa kwa maziko kesho. 



Mmoja wa wanafamilia akibugujikwa na machozi wakati wa 

shughuli hiyo ya kuuaga mwili, Viwanja vya Karimjee jijini Dar es 

Salaam leo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia, Dk. 

Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Spika wa 

Bunge, Anne Makinda, Jaji Mkuu Kiongozi, Fakhi Jundu na Jaji 

Mkuu, Mohamed Chande Othmani, wakiwa katika shughuli hiyo, 

ya kuuaga mwili huo.

No comments:

Post a Comment