TANGAZO


Tuesday, February 5, 2013

Kikao kazi cha Maofisa Habari wa Serikali, Mjini Dodoma, chaingia siku ya pili, Changamoto mbalimbali zaibuliwa

Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy, akiwasilisha mada kuhusu mkakati wa Mawasiliano wakati wa Kikao kazi cha Maofisa Habari wa Serikali kinachoendelea mjini Dodoma leo. (Picha zote na Aron Msigwa –MAELEZO)
Baadhi ya Maofisa Habari wa Serikali, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Peter Millanzi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Midradji Maez, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Shirika la Reli Tanzania (TRL) na Abel Ngapemba, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).
Maofisa Habari kutoka Wilaya na Mikoa, mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha Maofisa Habari mjini Dodoma, wakiwa katika majadiliano ya pamoja kuhusu mafanikio na changamoto zinzoyakabili maeneo yao ya kazi.

Maofisa Habari kutoka Wizara mbalimbali, waliohudhuria kikao kazi cha maofisa habari mjini Dodoma, wakiwa katika majadiliano ya vikundi kuhusu mafanikio na changamoto zinazoyakabili maeneo yao, ya kazi, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kikundi hicho, Luteni Kanali Juma Sipe, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Serikalini, Wizara ya Ulinzi. 

Na Aron Msigwa, Dodoma

5/2/2013, 

Kikao kazi cha Maofisa Habari wa Serikali kutoka Wizara, taasisi, 

Wakala wa Serikali, Mashirika ya umma, Mikoa na Wilaya 

mbalimbali nchini leo, kimeingia siku ya pili mjini Dodoma kwa  

maofisa hao kupata fursa ya kujadili changamoto zinazokabili 

vitengo vya  habari na mawasiliano serikalini na namna ya 

kuzitatua.

Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo ile 

ya Mwongozo wa Ofisi za Mawasiliano serikalini iliyowasilishwa 

na Mkurugenzi wa Msaidizi kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) 

anayeshughulikia uratibu wa vitengo vya mawasiliano serikalini 

akitoa msisitizo mkubwa  kwa maafisa habari kuyafahamu vizuri 

majukumu yao ya kazi kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa 

umma ili kuboresha utendaji wa kazi.

Pia maafisa hao wamepata fursa ya kujifunza namna ya kuboresha  

mawasiliano serikalini kupitia mada ya mkakati wa mawasiliano 

(Communication Strategy) wa kuiwezesha jamii kupata taarifa 

sahihi kwa muda muafaka ,mada iliyowasilishwa na Meneja 

mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) 

Bw. Innocent Mungy.

Katika mada hiyo Bw. Mungy ametoa wito kwa maafisa hao 

kuzitumia nafasi zao kutoa taarifa kwa umma mara kwa mara ili 

kuwapa fursa wananchi kufahamu yale yanayofanywa na 

serikalini.

Ametoa wito maafisa hao kushirikiana na vyombo mbalimbali vya 

habari katika kutekeleza mkakati huo kwa kuhakikisha kuwa 

wanatoa habari kwa umma kupitia radio, magazeti, televisheni na 

mitandao ya kijamii ili kuepusha madhara yanayoweza 

kusababishwa na jamii kukosa taarifa sahihi za serikali za 

utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo.

No comments:

Post a Comment