TANGAZO


Sunday, December 30, 2012

Waziri Mkuu Pinda ahimiza maendeleo jimboni Katavi

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akipatiwa maelezo na mtalamu wa Tanesco Makao Makuu Eng. Tumaini Temu kuhusu jinsi jenereta walilolifunga linavyofanya kazi katika kuzalisha umeme katika kijiji cha Kibaoni. kushoto kwa Waziri Mkuu ni tekinisheni wa Tanesco Bibi.Salama Mpera.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akikagua kibanda kilichojengwa kwa ajili ya kuweka jenereta la kufua umeme katika kijiji cha Kibaoni, Katavi. Waziri Mkuu yupo katika ziara ya kukukagua shughuli za maendeleo na mapumziko ya Krismasi na mwaka mpya kijijini kwao, Kibaoni Katavi.
 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akiwa katika shamaba lake katika kijiji cha Kibaoni, Katavi akiangalia mahindi yalivyostawi.
 
Godfrey Pinda, ambaye ni mdogo wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akimwelezea Waziri Mkuu kuhusu anavyolima kilimo cha mananasi na minazi katika shamba lake kijijini Kibaoni, Katavi. Waziri Mkuu yupo katika jimbo lake la Katavi katika kukagua shughuli za maendeleo pamoja na mapumziko ya Krismasi na mwaka mpya. (Picha zote na Chris Mfinanga)

No comments:

Post a Comment