![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjH2yUf2qOtn42JRDhxU-D1ODhJ_k67s26Kvbgc0TXzSZ5C1jS_ScolHbpNllEzt4g6tGZA1cfeScmmJGvOk2J9pTqWXYDAe_duWO1tjeQZU8S1OcqOdG_kYrdt63bkFy6oA4C-8uwKJY0/s640/1.+Vijana+Jazz,+Kulia+ni,+Saburi+Athumani+%28Kiongozi+wa+bendi%29,+Abdallah+Mgona+Hazelu+%28Katibu+wa+bendi%29,+Nuru+Mhina+%27Baby+Whiye%27+na+Roshi+Mselela,+wakiimba+ukumbi+wa+Masae+Bar,+Kawe.jpg)
Wanamuziki wa kundi hilo, wakizirudi ngoma, wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza ukumbi wa Masae Bar, Kawe jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa waimbaji wa kundi hilo, akiwajibika kwenye onesho hilo.
Mwimbaji Abdallah Mgonahazelu akiimba wakati wa onesho hilo.
Mwimbaji Nuru Mhina 'Baby White', akiimba wakati wa onesho hilo.
Mwimbaji Roshi, akiwa kazini katika onesho hilo, ukumbi wa Masae Bar, Kawe jijini.
Mpuliza Sexaphone (mdomo wa bata), akiwajibika jukwaani katika onesho hilo.
DAR ES SALAAM, Tanzania
BAADA ya kuwa
'juu ya mawe' kwa muda mrefu, bendi ya muziki wa dansi ya Vijana Jazz, 'Wana
Air Pambamoto', imeibuka upya kuanza kupiga muziki kwenye kumbi za starehe, huku
ikiwa ikiipua vibao viwili vipya, kusuuza nyoyo za mashaki wake.
Ikipiga kwa
mara ya kwanza kwenye ukumbi wa Masae Bar, Kawe Wilaya ya Kinodoni, jijini Dar es
Salaam, usiku wa kuamkia leo, bendi hiyo, imedhihirisha kwamba bado ni moto wa kuotea mbali na kwamba mashabiki wake
wengi bado wapo.
Ikitumbuiza kwenye ukumbi
huo, unaotazamana na kilichokuwa kiwanda cha kusindika nyama cha Tanganyika
Packes, Vijana Jazz ilithihirisha kuwa 'bado wamo', kwa kupiga nyimbo zake za
zamani zikiwemo 'Mary Maria', 'Mwsiho wa mwezi', 'Ngapulila' na 'mawifi',
zilizopigwa enzi za muasisi wa bendi hiyo, marehemu Ahmed Maneti katika miaka
ya 1980.
Nyimbo hizo,
ziliwapeleka puta mashabiki wa bendi hiyo na kuwafanya kucheza kwa hamasa kubwa huku baadhi yao
wakifuatisha kuimba sambamba na wanamuziki waliovuokuwa wakiimba jukwaani na
wengine kwenda jukwaani kutuza waimbaji.
Licha ya
kuonyesha kuwa bendi hiyo bado ni mahiri, wanamuziki wa zamani iliobaki nao ni
Roshi Mselela, Nuru Mhina (Baby White) na viongozi wa bendi Abdallah Mgonahazelu
(Katibu) na Saburi Athuman ambaye ni kiongozi wa bendi.
Vibao vibya
ambavyo bendi hiyo imeipua ni 'Utanieleza nini', utunzi wake kiongozi huyo na
Kina mama wanaweza uliotungwa na Mgonahazelu.
Athumani
alisema, nyumbo hizo zimesharekodiwa na hivi karibuni zitaanza kuingizwa sokoni,
lakini akasema bendi yake itafanya hivyo baada ya kuzipiga mara nyingi
majukwaani na kuzoeleka masikioni kwa mashabiki wao.
Alisema wakati
kazi ya kuzirekodi nyimbo hizo kwa ajili ya kiusikilizwa, imeshakamilika, sasa
bendi imo katika jitihada za kuzirekodi katika video ili ziweze kurushwa kwenye
vipindi vya Televisheni na pia kuuzwa kwa mashabiki.
"Tunamshukuru
Rais Jakaya Kikwete ametutoa juu ya mawe, hivi vyombo mnavyoona ametuwezesha
mheshimiwa Kikweye. Kwa kweli tunamshukuru sana", alisema Mgonahazeru wakati
kabla ya bendi hiyo kuanza kuiba wimbo wao mpya wa 'Utanieleza
nini'.
Vijana Jazz ni
moja ya bendi ambazo Mratibu wa Budurano zote kwenye ukumbi huo wa Masae, Juma
Mbizo, amesema atakuwa anazitumia kutoa burudani kwa mashabiki. Nyingine ni kama
Msondo Band na FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma'.
No comments:
Post a Comment