TANGAZO


Tuesday, November 13, 2012

Washiriki wa maandalizi ya Tamasha la Azaki za Kiraia, wataka Katiba ijayo iandikwe kwa Kiswahili


Bi. Zippora Shekilango ambaye ni mwasisi  wa mtaa wa Shekilango jijini Dar es Salaam, akichangia mada leo katika ukumbi wa Ubungo Plaza juu ya Kiswahili kutumika kama lugha ya Taifa katika katiba ijayo, wakati wa warsha ya maandalizi ya Tamasha la Azaki za Kiraia Tanzani litakalo anza  kesho jijini.  (Picha na Francis Godwin)

Na Francis  Godwin
WASHIRIKI wa Azaki   za  kiraia Tanzania wamependekeza katiba ijayo  kuhakikisha lugha ya Kiswahili inakuwa ni lugha ya Taifa badala ya kuendelea  kuliingiza Taifa katika utumwa wa  kutumia lugha ya kiingereza .

Kwani   wamedai  kuwa lugha ya kigeni  ndio imekuwa ikizidi  kuwapa mwanya  wageni na  watu  wachache  wanaofahamu  vema lugha ya kiingereza  kujinufaisha na raslimali za Taifa kwa mikataba  isiyoeleweka kwa wananchi  wasioelewa  lugha hiyo ya kiingereza.

  Akichangia mada juu ya mtazamo  wa azaki za kiraia kuhusu elimu ya Tanzania leo, wakati wa mafunzo ya  siku  mbili  ya maandalizi ya tamasha la mwaka la azaki za kiraia warsha inayoendelea  katika  ukumbi  wa  Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam  Zippora Shekilango ambaye ni mwasisi  wa mtaa wa Shekilango jijini Dar es Salaam. 

Alisema  kuwa wakati  baadhi ya nchi  dunia kama China na Uingereza wananufaika na lugha  za mataifa  yao katika  kukuza ajira na kuongeza  kipato  cha Taifa  kwa  kuwa na  wakalimani  wengi  wa lugha ya kwao ,Tanzania tumeendelea kujitumikisha  kwa  kuikumbutia lugha ya kigeni na kuipa mgongo lugha  ya kishwahili ambayo ni lugha yetu .

Hivyo  alisema lazima sasa Tanzania  kusimama imara katika kutetea lugha  yetu ikiwa ni pamoja na kuwa ni lugha ya kufundishia mashuleni badala ya  kutumia lugha ya kiingereza kama ni lugha ya  kufundishia  mashuleni.

Hivyo  alitaka katika katiba ijayo  kuhakikisha suala la lugha ya Kiswahili kupewa  kipaumbelea zaidi japo wananchi  hawatazuiwa  kujifunza  lugha  nyingine huku Kiswahili  kikibaki kama ni lugha ya Taifa  na si vinginevyo.

Mshiriki  kutoka  kundi la  vyombo  vya habari  Tanzania Henry Muhanika  alisema  kuwa  ili kuhakikisha  lugha ya Kiswahili  linapewa kipaumbele katika Taifa  ni  vema kuingizwa rasmi katika katiba ijayo  ili kuenzi utamaduni  wetu.

Hivyo alisema lazima kuwekeza  zaidi katika utamaduni  wetu kama  watanzania  kwa  kutumia  lugha  yetu ya  Kiswahili badala ya  kuendelea  kukubali  kuwa  watumwa katika Taifa kwa  kuipa nafasi lugha ya  kigeni  katika Taifa  huru.

Kwa upande  wake mkurugenzi   wa chama cha  waandishi  wa habari  wanawake Tanzania (TAMWA),Valeria Msoka alisema  kuwa ni  vema katiba  ijayo kutamka  wazi  juu ya Kiswahili  kuwa ni lugha ya Taifa .

Alisema  kuwa serikali ni lazima  kuweka msukomo  wa kipekee katika kuwekeza zaidi katika lugha ya Kiswahili ili kujinasua na utumwa wa  kutumia lugha  za kigeni zaidi.

Kwani  alisema inashangaza  kuona Tanzania ikiendelea  kukumbatia  lugha ya kigeni  wakati baadhi ya nchi  zikikwepa  kutumia lugha  hiyo ya kiingereza.
Katika hatua nyingine Msoka alipendekeza kuwa katiba ijayo mbali ya lugha ya Kiswahili  kupewa kipaumbele bado suala la kijinsia katika katiba ijayo ni lazima kupewa kipaumbele zaidi.


No comments:

Post a Comment