TANGAZO


Saturday, November 10, 2012

Walter Chilambo aibuka mshindi wa EBSS 2012

 Mshindi wa Shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), Walter Chilambo akikabidhiwa sanduku lenye kitita cha shilingi milioni 50 baada ya kuibuka mshindi katika shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Washindi wengine ni mwanadada Salma Abushiri  (Zanzibar), aliyeshika nafasi ya pili na watatu ni Wababa Mtuka wa Dar es Salaam.
Mshindi wa Shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), Walter Chilambo, akifurahia zawadi yake baada ya kukabidhiwa usiku wa kuamkia leo, ukumbi wa Diamond Jubillee, Dar es Salaam. 

Baadhi ya mashabiki wa mshindi wa shindano hilo la EBSS,Walter Chilambo wakishangilia kwa shangwe na vifijo mara baada kutamkwa yeye ndiye kinara katika kilele cha shindano hilo lililovuta hisia za watu wengi.

Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, na Jaji Mkuu wa Shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), akiwa amemkumbatia mshindi wa shindano hilo Walter Chilambo ndani ya ukumbi wa Diamond,Chilambo ameibuka na kitita cha shilingi Milioni 50.

Msanii Barnaba akiimba na mmoja wa washiriki wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS).

Mshiriki wa EBSS NshomaNg'hangasamala akiimba moja ya wimbo wake jukwaani.

Mwanadada Salma Albushiri akiimba kwa hisia huku akipiga gitaa mbele ya mashabiki wake waliofika kumshuhudia ndani ya ukumbi wa Diamond.

Mapouda.! majaji hawaishi vituko. (Picha zote kwa hisani ya Habari Mseto na Father Kidevu Blog)

No comments:

Post a Comment