TANGAZO


Tuesday, November 6, 2012

Subash Petel, Asas na Yusuf Manjia waonyesha njia ya kuchangia ujenzi wa mabweni wilaya ya Kilolo

Mkuu wa wilaya ya  Kilolo mkoani Iringa, Gerald Guninita (kushoto), akimkabidhi msaada wa bati 300 zenye thamani ya  zaidi ya shilingi milioni 8, Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Kilolo, Mohamed Gwalima jana.Mkuu huyo wa Wilaya alikabidhi msaada  huo, wa bati baada ya  kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya  M.M Instegrated Steel  Mills ya jijini Dar es Salaam, Subash Petel kwa  ajili ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya  watoto  wa  kike Wlaya hiyo ya Kilolo. (Picha, Habari na Francis Godwin)


Na  Francis Godwin,Iringa

BAADA ya mfanyabiashara na kada wa chama  cha mapinduzi (CCM)  mkoa  wa Iringa  Salim Abri Asas kukabidhi mifuko 200 ya saruji yenye thamani ya zaidi ya shilingi  milioni 3 ,mfanyabiashara maarufu nchini  Subash Patel  ameungana na  Asas kwa  kuunga mkono jitihada za   mkuu  wa wilaya ya  kilolo katika mkoa  wa Iringa Gerald Guninita  kwa  kwa  kuchangia bati 300 zenye thamani ya zaidi ya  shilingi milioni 8 ili  kusaidia kukamilisha  ujenzi huo wa mabweni zaidi ya 8 yanayoendelea katika  wilaya hiyo

Petel ambaye ni mkurugenzi mtendaji  wa kampuni ya  M.M.mechangia  bati hizo kama njia ya  kuunga mkono  jitihada za  kunusuru  elimu kwa mtoto  wa  kike  wilaya ya  Kilolo na uboreshaji  wa elimu wilaya  hiyo mpya  ulioanzishwa na mkuu  wa wilaya ya Kilolo Bw Guninita.

Mfanyabiashara  huyo ameeleza  kuguswa na  jitihada hizo zinazofanywa na serikali ya  wilaya ya Kilolo  kupitia mkuu  wa wilaya  hiyo katika kumsaidia mtoto  wa  kike kupata  elimu bila kurubuniwa na  watu wasiopenda maendeleo ya  watoto hao kwa  kuwakatisha masomo kwa  kuwapa ujauzito.

Hivyo  alisema  kuwa  ili  kusaidia ujenzi huo  kampuni yake imelazimika  kuchangia  bati hizo 300 ili kusaidia  kuezeka baadhi ya mabweni ambayo  ujenzi  wake  utakuwa  umekamilika .

Akikabidhi msaada  huo   jana  kwa  mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri ya  wilaya ya  Kilolo  Momahed Gwalima   kwa niaba ya mfanyabiashara Patel mkuu  wa  wilaya ya Kilolo  Bw. Guninita  alisema  kuwa  bati hizo 300 zimetolewa na mfanyabiashara  huyo baada  ya  ofisi yake  kutuma barua ya maombi  kwa mfanyabiashara   huyo na  wengine .

Guninita  alisema  kuwa kati ya majukumu aliyonayo katika   wilaya  hiyo ya Kilolo ni kuhakikisha anasaidiana na  wananchi  wa  wilaya  ya Kilolo pamoja na wadau mbali mbali  wa maendeleo katika  kusukuma mbele  gurudumu la maendeleo ya  wilaya  hiyo ambayo katika mkoa  wa Iringa ni wilaya  pekee  ambayo bado ipo nyuma kwa  elimu.

Kwani  alisema kuwa  mbali ya  wilaya  hiyo ya  Kilolo kuwa ni  wilaya  ina fursa mbali mbali za kimaendeleo ila  bado katika  sekta ya  elimu  hasa katika suala la mabweni ya  wanafunzi  ,kilolo ipo nyuma na kuwa kupitia mkakati huo  ulioanzishwa wa ujenzi  wa mabweni na vyumba vya madarasa  wilaya  hiyo  itapiga hatua  zaidi katika sekta  hiyo ya  elimu.

Mkuu  huyo  wa  wilaya  alisema  kuwa  mbali ya  wilaya  hiyo  kuwa na  shule zaidi ya 10  za  sekondari  ila bado wilaya  hiyo inachangamoto kubwa ya Hosteli za watoto  wa  kike na hivyo kuanza ujenzi  wa Hosteli katika shule ya   sekondari  mbali mbali  wilayani  humo.

Bw Guninita  alisema  kuwa  kwa   sasa  shule ambazo zitanufaika na msaada  huo ni pamoja na  sekondari ya Uhambingeto,Gangwa ,Ukwega na Masisiwe  na kuwa  jitihada  zaidi  zinaendelea  kufanyika  ili  kuwafikia  wadau mbali mbali  wa   maendeleo katika  wilaya  hiyo  ili  kuweza kufanikisha harambee  hiyo ya  ujenzi  wa mabweni na Hosteli katika  wilaya ya Kilolo.

Pamoja na kumshukuru mfanyabiashara Petel kwa msaada wake  huo wa bati 300 bado  alimshukuru mfanyabiashara  Asas wa mkoani Iringa kwa  kuchangia  mifuko ya  saruji 200 pamoja na mfanyabiashara  Yusuf Manji ambae ni mkurugenzi wa Quality Group  kwa kuchangia  fedha  kiasi cha shilingi 500,000 kwa njia ya  hundi kwa ajili ya  maendeleo ya  elimu  wilaya  hiyo ya  Kilolo na kuwaomba  wadau  wengine  kuendelea  kuchangia zaidi.

Kwa  upande  wake  mkurugenzi  wa Halmashauri ya  wilaya ya  Kilolo Bw Ngwalima  alimpongeza mkuu  huyo  wa wilaya  kwa jitihada za muda mufupi ambazo amezionyesha katika  wilaya  hiyo ya Kilolo na  kuwa mkuu  huyo wa wilaya  mbali ya  kuwa bado hajapata  kumaliza hata mwaka mmoja tangu alipoteuliwa na Rais Jakaya  Kikwete  ila mambo ambayo amekuwa akiyafanya katika  wilaya  ya Kilolo ni makubwa na anapaswa  kupongezwa kwa utendaji wake kazi.

No comments:

Post a Comment