TANGAZO


Tuesday, November 20, 2012

Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilal azindua mpango wa Afya ya macho kwa mtoto kwa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda jijini Dar es Salaam leo

Wasanii wa kundi la 7 Blind, wakitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa kuboresha Afya ya Macho kwa mtoto, ujulikanao kwa jina la Seeing is Believing, kwa nchi za Tanzania, Kenya na Ugada, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Gharib Mohamed Bilal(kushoto), akisalimiana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Agrey Manry, mara baada ya kuwasili viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kuzinduza awamu ya uboreshaji wa huduma ya Afya ya macho kwa mtoto, Dar es Salaam leo.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Gharib Mohamed Bilal(kushoto), akisalimiana na viongozi wa Wilaya, mara baada ya kuwasili viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kuzindua awamu ya uboreshaji wa huduma ya Afya ya macho kwa mtoto, Dar es Salaam leo.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Gharib Mohamed Bilal(kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Gabriel Fuime, mara baada ya kuwasili viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kuzindua awamu ya uboreshaji wa huduma ya Afya ya macho kwa mtoto, kwa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, Dar es Salaam leo.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Gharib Mohamed Bila, akiweka saini kitabu cha wageni, mara baada ya kuwasili viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kuzindua awamu ya uboreshaji wa huduma ya Afya ya macho kwa mtoto, kwa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, Dar es Salaam leo.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akipatiwa maelezo  na Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Kukinga upofu kwa nchi za Afrika, Kovin Naidoo (kushoto) kuto, wakati alipotembelea mabanda kwa ajili ya kujionea shughuli za upimaji macho kwa watoto, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’, maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, uliodhaminiwa na Benki ya Standard Chartered, Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal (wa pili kushoto), akipatiwa maelezo na Mwakilishi wa taasisi ya Brian Holden Istitute, Mary Wepo (kulia), wakati alipotembelea mabanda kwa ajili ya kujionea shughuli za upimaji macho kwa watoto, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’, maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, uliodhaminiwa na Benki ya Standard Chartered, Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012.
 
Watoto wakijiorodhesha kwa ajili ya kupima maradhi ya macho wakati wa uzinduai wa mpango huo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo.
 
Daktari Bingwa wa macho kwa Watoto, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, ‘Optometrist’, Judith Mwende, akimpima macho mtoto Abubakari Sihaba Kaimu, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Daktari Bingwa wa macho kwa Watoto, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, ‘Optometrist’, Judith Mwende, wakati Makamu alipokuwa akitembelea katika Mabanda kujionea shughuli za upimaji macho kwa watoto, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012. 

Daktari Bingwa wa macho kwa Watoto, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, ‘Optometrist’, Judith Mwende (kushoto), akimpima macho mtoto Abubakar Sihaba Kaimu, mkazi wa Keko Mwanga, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012. Anayemsaidia ni Mratibu wa huduma za upimaji macho, Dk. Magdalena Ponera na kushoto ni Dk. Celina Mhina.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa  Daktari Bingwa wa macho kwa Watoto, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, ‘Optometrist’, Judith Mwende, wakati Makamu alipokuwa akitembelea katika Mabanda kujionea shughuli za upimaji macho kwa watoto, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012.  Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Agrey Manry, (wa tatu kushoto) ni Mtoto Abubakar Sihaba Kaimu, mkazi wa Keko Mwanga, akipimwa macho. (Picha na OMR)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa  Dkt. Paulina Mvella, wakati akimpima mtoto, Brayan Paul (7) mkazi wa Kigamboni, wakati Makamu alipokuwa akitembelea katika Mabanda kujionea shughuli za upimaji macho kwa watoto, wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, uliodhaminiwa na Benki ya Standard Chartered, uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012.  Wa pili kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Agrey Manry.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mpango wa miaka mine wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, uliodhaminiwa na Benki ya Standard Chartered, uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini maalum ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Mpango wa miaka minne wa ‘Kuona ni Kuamini’ maalum kwa ajili ya kuboresha afya ya macho kwa watoto kwa Nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, uliodhaminiwa na Benki ya Standard Chartered, uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo Nov 20, 2012.


Shughuli ya upimaji wa macho kwa watoto, ikiendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, wakati wa uzinduzi wa mpango huo, leo. 

No comments:

Post a Comment