TANGAZO


Sunday, September 23, 2012

Meya wa Ilala, Jerry Slaa akabidhi kisima cha maji na vifaa vya michezo kwa wakazi Gongo la Mboto


Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akichota maji kwenye kisima alichokikabidhi kwa wakazi wa mtaa wa Kilimo, Kata ya Gongo la Mboto kama ishara ya kukizindua rasmi, huku baadhi ya viongozi na wakazi wa mtaa huo wakishuhudia.
 
Meya wa Ilala, Jerry Silaa akimkabidhi seti ya vifaa vya michezo, mmoja kati ya manahodha wa timu zilizoshiriki ligi ya mpira wa miguu katika kata ya Gongo la Mboto, ijulikanayo kama Jerry Super 8.
 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, ambaye pia ni diwani wa kata ya Gongo la Mboto, akizindua rasmi kisima cha maji kilichojengwa kwa ushirikiano wake na mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Kilimo, Moshi Mwaluko.
 
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Gongo la Mboto, wakimsikiliza kwa makini Diwani wa kata yao, Meya wa Ilala, Jerry Silaa (hayupo pichani), wakati akiwakabidhi vifaa vya michezo pamoja na kisima cha maji. (Picha zote na mdau wetu)

No comments:

Post a Comment