TANGAZO


Saturday, June 23, 2012

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mgulani watembelea yatima wa DonBosco

Watoto wanaolelewa katika kituo cha yatima cha Friends of Don Bosco kilichopo Kimara jijini, Dar es Salaam, wakifurahia zawadi za miswaki na dawa za meno za Whitedent walizopewa na wanafunzi wenzao kutoka shule ya msingi Mgulani waliowatembelea kituoni hapo hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya kufamiana zaidi katika maendeleo ya elimu kwa ujumla.


Mwnafunzi wa darasa la saba kutoka shule ya msingi Mgulani Emmanuel George (kulia) akiwapa zawadi ya mpira wanafunzi wenzake ambao ni yatima wanaolelewa katika kituo cha Friends of DonBosco kilichopo Kimara pindi walipotembelea kituo hicho hivi karibuni chini ya uwakilishi wa Chemi & Cotex ltd.

Piscus Laswai ambaye pia ni mmoja wa yatima wanaolelewa na kituo cha Friends of DonBosco kilichopo Kimara jijini akipokea zawadi ya taa zinazotumia mwanga wa jua kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi Mgulani ambazo zitawasaidia yatima hao kujisomea hasa nyakati za usiku kunapokua na tatizo la umeme.

Watoto yatima wanaoishi kituo cha Friends of DonBosco kimara jijini wakiwakaribisha wanafunzi kutoka shule ya msingi Mgulani kituoni hapo pindi walipokuja kuwatembelea yatima hao na kufahamiana zaidi hasa kielimu pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka kampuni ya Chemi & cotex. (Picha zote na mpigapicha wetu)

No comments:

Post a Comment