TANGAZO


Thursday, June 21, 2012

Rais Kikwete atembelea shamba la mfano kijiji cha Chikopelo, Bahi, Dodoma

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua  nyanya  na mazo mengine ya mboga pamoja na mizabibu katika shamba linalomilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade huko katika kijiji cha Chikopelo,wilaya ya Bahi, Mkoani Dodoma  leo asubuhi.Kushoto ni mmoja wa wamiliki wa Shamba hilo Bwana Alon Hoven anayeshirikiana na Bwana Dunstan Mrutu(hayupo pichani).shamba hilo linamwagiliwa kwa kutumia teknolojia ya  matone(Drip irrigation system). wakati wa ziara yake hiyo leo. (Picha na Freddy Maro)

Mmoja wa Wamiliki wa Shamba la Mboga katika kijiji cha Chikopelo, Alon Hoven kimwonesha Rais Jakaya Mrisho Kikwete, baadhi ya mazao yanayozalishwa kwa kutumia mbegu bora pamoja na teknolojia ya umwagiliaji wa matone wakati Rais alipotembelea shamba hilo katika kijiji cha Chikopelo, wilayani Bahi, mkoani  Dodoma leo asubuhi. Shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mia moja linamilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade chini ya Dunstan Mrutu na Alon Hoven raia wa Israel.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Rais Kikwete alisifu juhudi za wawekezaji hao kwa kutumia mbinu za kisasa za kilimo na kuwaasa wanakijiji wa Chikopelo kujifunza mbinu bora za kilimo hicho cha mboga ili waweze kupata ufanisi na kuboresha maisha yao. Rais Kikwete alitumia fursa hiyo kuwaonya viongozi wa kijiji cha Chikopelo kutoendelea kuuza ardhi yote kwa wawekezaji na badala yake kutunza na kuilinda kwaajili ya kizazi kijacho.

Awali katika salamu zao kwa Rais,bBwana Dunstan Mrutu  na mmiliki mwenzake, Alon Hoven mbali na kutoa ajira kwa wanakijiji hao waliahidi kushirikiana nao katika kujifunza mbinu bora za kilimo na kuwawezesha kuzalisha mazao bora na mengi.

Mmoja wa Wamiliki wa Shamba la Mboga katika kijiji cha Chikopelo, Alon Hoven kimwonesha Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiangalia baadhi ya mazao yanayozalishwa kwa kutumia mbegu bora pamoja na teknolojia ya umwagiliaji wa matone, shamba linalomilikiwa kwa pamoja na  Kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade chini ya Dunstan Mrutu na Alon Hoven, raia wa Israel. 


No comments:

Post a Comment