TANGAZO


Wednesday, May 2, 2012

Rais wa Zanzibar, Dk. Shein aanza ziara ya Kaskazini Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati), akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Pembe Juma Pembe (kulia), wakati alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Amali, Mkokotoni akiwa  katika ziara ya Mkoa huo iliyoanza leo. (Picha na Ramadhan Othman, Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (wa tatu kushoto), akipata taarifa ya utekelezaji wa kazi za  Mkoa wa Kaskazini Unguja, iliyosomwa na Maalim Maulid Nafasi Juma, leo katika  ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni, akiwa katika ziara ya kuangalia maendeleo ya  miradi mbalimbali ya kijamii katika Mkoa huo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akipokea  taarifa ya utekelezaji wa kazi za  Mkoa wa Kaskazini Unguja, kutoka kwa Mkuu wa Mkoa  huo, Pembe Juma Pembe, leo katika  ukumbi wa Chuo cha Amali, Mkokotoni akiwa katika ziara ya kuangalia maendeleo ya  miradi mbali mbali ya kijamii mkoani humo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati), akizungumza na viongozi na watendaji wa Wilaya ya Kaskazini B, ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni, akiwa  katika ziara. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Mwinyihaji Makame, kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais  Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haji Omar Kheir na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Pembe Juma Pembe.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua pazia kama ishara ya uwekaji wa jiwe la msingi wa madasrasa mapya katika Shule ya Matemwe, Kigomani leo, alipokuwa katika ziara ya Wilaya ya Kaskazini B, Unguja leo,  Mkoa wa Kaskazini, kuangalia maendeleo ya  miradi mbalimbali ya kijamii mkoani humo.


 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamuhuna, akizungumza na wananchi wakati alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ili awasalimie Wananchi wa Matemwe Kigomani na kutoa nasaha zake wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la madarasa mapya katika Shehia hiyo,calipokuwa katika ziara ya kuangalia maendeleo ya miradi mbalimbali ya kijamii Wilaya ya Kaskazini A.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na  Wananchi wa Matemwe Kigomani na wakati alipokuwa akitoa nasaha zake wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi madarasa mapya katika Shehia hiyo, alipokuwa katika ziara hiyo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na  Wananchi wa Matemwe Kigomani katika ziara yake hiyo, mkoani humo leo. 


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi wa Bwekunduni, baada kuizindua barabara ya kifusi katika shehia hiyo leo, alipokuwa katika ziara ya Mkoa wa Kaskazini Unguja, kuangalia maendeleo ya miradi mbalimbali ya kijamii katika wilaya ya Kaskazini A.

No comments:

Post a Comment