TANGAZO


Saturday, April 28, 2012

Maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya Tanzania

 Baadhi ya washiriki maandamano ya kuadhimisha Wiki ya Wataalamu wa Afya nchini, wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali wakati wa maandamano yao, yaliyoanzia Hospitali ya Amana, jijini Dar es Salaam na kumalizikia viwanja vya Mnazi Mmoja, zilipofanyika sherehe hizo. (Picha zote na Khamisi Mussa)


Kikosi cha Jeshi la Polisi kikiongoza maandamano ya maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara ya Afya nchini leo, Aprili 28, jijini Dar es Salaam.






 Waandamanaji wakiwa na bango lao lenye ujumbe wa Huduma bora za Afya na mengineyo.




 Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya nchini, Dk. Ayoub Mgimba (kushoto), akikaribishwa na Katibu wa Mtendaji wa Chama cha Wataalamu wa Maabara Tanzania, Lilian Shija.




 Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya nchini, Dk. Ayoub Mgimba (katiakti), akiwa na Viongozi wa Chama cha Wataalamu wa Maabara Tanzania, wakipokea maandamano ya Wanataaluma wa Maabara, wakati wa maadhimisho hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. 



 Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya nchini, Dk. Ayoub Mgimba (katiakti), akiwa na Viongozi wa Chama cha Wataalamu wa Maabara Tanzania, wakipokea maandamano ya Wanataaluma wa Maabara, wakati wa maadhimisho hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa Mtendaji wa Chama cha Wataalamu wa Maabara Tanzania, Lilian Shija.


 Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya nchini, Dk. Ayoub Mgimba, akihutubia Wanataaluma wa Maabara Tanzania, wakati wa maadhimisho ya Wiki yao leo asubuhi, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.





 Wataalamu wa Maabara za Afya Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Dk. Ayoub Mgimba, mara baada kuwahutubia wataalamu hao kwenye maadhimisho ya Wiki ya Wataalamu wa Maabara za Afya nchini leo.




 Baadhi ya Wanataaluma wa Maabara za Afya Tanzania, wakiangalia baadhi ya vifaa vya kazi, wakati wa maadhimisho hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.




Mmoja wa washiriki na mtaalamu mwanafunzi wa Huduma za Maabara nchini, akishangaa matukio yaliyokuwa yakitokea kwenye maadhimisho hayo.
Baadhi ya wanafunzi wa Taalama ya Huduma za Maabara nchini wakiwa katika picha ya pamoja kwa ajili ya kuweka kumbukumbu za maadhimisho hayo.

No comments:

Post a Comment