TANGAZO


Tuesday, March 20, 2012

Rais Kikwete, azindua Ujenzi wa Ushirika Tower

 

Mchoro wa Jengo jipya la Ushirika Towers linalojengwa mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, linavyoonekana pichani. (Picha Zote na Richar Mwaikend)

Rais Jakaya Kikwete akifunua pazia ili kuweka jiwe la msingi wa ujenzi wa jengo hilo linalomilikiwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC).

Rais Jakaya Kikwete, akikabidhiwa zawadi na Balozi wa China nchini, wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa jengo hilo linalojengwa na kampuni ya China.

Rais Jakaya Kikwete, akizungumza na baadhi ya viongozi wa Taasisi za Fedha zilizoikopesha TFC kujenga jengo hilo.

Rais Jakaya Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa TFC pamoja na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa jengo la Ushirika Tower.

Wana Ushirika wakiwa na furaha walipokuwa wakiandamana mbele ya Rais Kikwete wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa jeng la Ushirika Tower na maadhimisho ya mwaka wa Kimataifa wa Ushirika Duniani, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo.

Baadhi ya washirika wakipita na kupung mikono kwenye maandamano ya kuadhimisha siku ya washirika nchini.


Washirika wakiwa wamenyanyua juu mabango yenye ujumbe mbalimbali wakati wa maandamano yao leo.

Baadhi ya wadau na wanaushirika wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete, wakati alipokuwa akiwaahutubia kwenye maadhimisho hayo.
 

Bendi ya DDC Mlimani Park, ikitumuiza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ushirika nchini.

No comments:

Post a Comment