TANGAZO


Tuesday, March 27, 2012

Mbaguzi wa Muamba kwenda jela


Liam stacey
Mahakama ya Uingereza imemfunga jela mwanafunzi aliyeweka ujumbe wa kibaguzi uliomkejeli Fabrice Muamba katika mtandao wa Twiteer. Mcheza soka huyo alizirahi baada ya moyo wake kusimama wakati akichezea klabu yake mapema mwezi huu.
Liam Stacey amekiri kuchochea chuki za rangi ambapo amesukumwa jela siku 56. Muamba amepata nafuu japo yungani katika chumba cha wagonjwa mahututi. Mchuano wa FA kati ya klabu yake ya Bolton na Tottenham ambao ulisimamishwa baada yake kuzirahi unachezwa tena leo usiku.

No comments:

Post a Comment