TANGAZO


Wednesday, February 1, 2012

Mkataba wa kuyaondoa makontena bandarini wasainiwa

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA), Ephraim Mgawe (kulia) akimkabidhi Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA), Stephen Ngatunga hati ya makubaliano ya kusaidia kupunguza msongamano wa makontena katika bandari ya Dar es Salaam kwa kuyahamishia katika Bandari Kavu. Hafla hiyo ilifanyika eneo la Bandari hiyo leo, ambapo taasisi nyingine nne zilipata hati hizo. (Picha na Richard Mwaikenda)

Naibu Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Patrick Kisaka (kushoto) akipokea hati hiyo, kutoka kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA), Ephraim Mgawe (kulia) katika hafla hiyo.
 
 
Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya Tanzania Road Haulage (1980) LTD, Ali Hussein Lilan akipokea hati hiyo kutoka kwa Mgawe.

Katibu Mkuu wa Mawakala wa Meli Tanzania (TASAA), Peter Kirigini (kushoto), akipokea hati kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA), Ephraim Mgawe (kulia) katika hafla hiyo.

Baadhi ya wageni waalikwa wakishuhudia makabidhiano hayo.
 
 
 
Viongozi hao wakitiliana saini mkataba huo katika hafla hiyo, iliyofanyika Dar es Salaam leo asubuhi.
 
 
 
Wakitiliana saini mkataba huo, bandarini Dar es Salaam leo.
 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TICTS, Nathan Bissett akikabidhiwa hati ya makubaliano na Mkurugenzi Mkuu wa THA, Mgawe.

No comments:

Post a Comment