Pages

Friday, January 20, 2012

Nape Mgeni rasmi mahafali ya Kidato cha sita, Sekondari ya Nsumba Mwanza





Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkabidhi cheti mhitimu wa kidato cha sita, Burilo Busagi, katika mahafali ya kidato cha sita shule ya Sekondari Nsumba, jijini Mwanza leo. Jumla ya wahitimu 374 wa kidato hicho walipewa vyeti. Kushoto ni Mkuu wa shule hiyo Josephat Zakeyo. 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkabidhi cheti mhitimu wa kidato cha sita, Tifugundulwa Tumbika katika mahafali ya kidato cha sita shule ya Sekondari Nsumba, Mwanza. Tumbika alikabidhiwa cheti hicho kwa kuibuka mwanafunzi bora katika kuzungumza Kiingereza. Wapili kulia ni Mkuu wa shule hiyo Josephat Zakeo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na mwanafunzi aliyesoma shule ya sekondari ya Nsumba, Mwanza, kati ya mwaka 1954 na 1957 (darasa la nane na kumi) Damas Ngoma, wakati wa mahafali ya kidato cha sita ya shule hiyo leo. Nape ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo alisoma pia katika shule hiyo hadi kidato cha nne mwaka ambako alimaliza mwaka 97. Watatu ni Mkuu wa shule hiyo Josephat Zakeo.(Picha na Bashir Nkoromo).

No comments:

Post a Comment