TANGAZO


Tuesday, January 31, 2012

Mwendesha pikipiki alipoponea tundu la sindano kupoteza maisha

Mwendesha pikipiki akiwa ameanguka chini kwenye barabara ya Kawawa, maeneo ya Ilala Boma, baada ya pikipiki yake kuteleza na kumdondosha chini, barabarani huku kofia ya kumkinga na ajali (helmet), ikiwa imevuka kichwani, hatua iliyomsababishia kuumia sehemu ya paji lake la uso, leo asubuhi. (Picha na Kassim Mbarouk)


  Mwendesha pikipiki akijaribu kujinyanyua baada ya kupata ajali ya kudondoka na pikipiki yake bila kuguswa na kitu chochote, kwenye barabara ya Kawawa, Dar es Salaam leo asubuhi, Ilala Boma.



 Wananchi wakijaribu kumsaidia kwa kumtafutia gari la kumpeleka hospitali kwa ajili ya kupatiwa huduma ya matibabu.



 Mwendesha pikipiki akiwa amelala bila kujitambua, huku wananchi wakitaka kumatia msaada, baada ya kupata ajali ya kudondoka kwenye pikipiki yake wakati akiwa kwenye barabara ya Kawawa, maeneo ya Ilala Boma, Dar es Salaam.


Wasamaria wema, wakimbeba kwa ajili ya kumwingiza kwenye gari la kumpeleka hospitali, kijana mwendesha pikipiki, aliyedondoka na kuumia sehemu ya paji lake la uso, kutokana na kuteleza kwa pikipiki hiyo, wakati akiiendesha maeneo ya Ilala Boma, barabara ya Kawawa, Dar es Salaam leo. (Picha na Kassim Mbarouk)

No comments:

Post a Comment