TANGAZO


Saturday, January 28, 2012

Boko Haram wauawa Nigeria


Jeshi la Nigeria linasema limewapiga risasi na kuwauwa wafuasi 11 wa kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu, Boko Haram, kaskazini-mashariki mwa nchi.

Watu waliouliwa na Boko Haram

Msemaji wa jeshi alieleza kwamba wapiganaji hao waliuwawa wakati wa mapambano katika mji wa Maiduguri, ambako kundi hilo lilianzishwa mwongo uliopita.
Juma lilopita watu kama 185 waliuwawa katika mji mwengine wa kaskazini, Kano, kwenye mashambulio kadha ya mabomu.
Boko Haram ilisema ilifanya mashambulio hayo, na imeonya kuwa itaendelea na ugaidi hadi mfumo wa sharia unafuatwa Nigeria nzima.

No comments:

Post a Comment