Pages

Saturday, March 12, 2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awapongeza wasanii wa filamu nchini

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura akimtambulisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama wapili kulia) wakati wa hafla ya kukabidhi Tuzo za Filamu kwa Waziri Mkuu Mhe. Majali K. Majaliwa (kushoto) jana jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFFA) Simon Mwakifamba (kulia) akimtambulisha msanii Elizabeth Michael (Lulu) wakati wa hafla kumkabidhi Mhe. Waziri Mkuu Tuzo walizoshinda nchini Nigeria jana, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa msanii wa Bongo Movie Single Mtambalike (Richie) wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jana jijini Dar es Salaam.Tuzo hiyo ya Africa Magic Viewers Choice ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili barani Afrika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akipokea Tuzo kutoka kwa msanii wa Bongo Movie Elizabeth Michael (Lulu) wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jana jijini Dar es Salaam.Tuzo hiyo ya Africa Magic Viewers Choice ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili barani Afrika.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akipokea Tuzo kutoka kwa msanii wa Bongo Movie Single Mtambalike wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jana jijini Dar es Salaam. Tuzo hiyo ya Africa Magic Viewers Choice. ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili baraniAfrika.
Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo wakifurahia jambo wakati wa hafla ya kumkabidhi Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majailiwa (hayupo pichani) Tuzo za Filamu za Africa Magic Viewers Choice kutoka kwa wasanii Single Mtambalike (Richie) na Elizabeth Michael (Lulu) jana jijini Dar es Salaam. Tuzo hizo ni Filamu Bora ya Lugha ya Kiswahili Barani Afrika aliyoshinda Single Mtambalike naFilamu Bora Afrika Mashariki kupitia filamu ya Mapenzi ya Mungu.
Mratibu wa Tamasha la Filamu la Tanzanite Said Assas akiwa pamoja na baadhi ya wasanii wakifuatilia hotuba ya Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa wakati wa hafla ya kumkabidhi Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majailiwa (hayupo pichani) Tuzo za Filamu za Africa Magic Viewers Choice kutoka kwa wasanii Single Mtambalike (Richie) na Elizabeth Michael (Lulu) jana jijini Dar es Salaam. Tuzo hizo ni Filamu Bora ya Lugha ya Kiswahili Barani Afrika aliyoshinda Single Mtambalike kupitia filamu ya “Kitendawili” na Filamu Bora Afrika Mashariki kupitia filamu ya Mapenzi ya Mungu.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa msanii wa Bongo Movie Elizabeth Michael (Lulu) katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Waziri Mkuu leo jijini Dar es Salaam.Anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura.Tuzo ya Africa Magic Viewers Choice ambapo amekuwa msanii bora wa Kike wa Afrika Mashariki kupitia filamu ya Mapenzi ya Mungu.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa msanii wa Bongo Movie Single Mtambalike (Richie) wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Waziri Mkuu leo jijini Dar es Salaam.Tuzo hiyo ya Africa Magic Viewers Choice ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili barani Afrika.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa akisalimiana na Mratibu wa Tamasha la Fila la Tanzanite Said Assaswalipokuta leo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa Tuzo kutoka kwa wasanii Single Mtambalike na Elizabeth Michael (Lulu).Tuzo hizo za Africa Magic Viewers Choice ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili barani Afrika huku Lulu akiibuka kuwa Msanii wa Kike Afrika Mashariki kupitia filamu ya Mapenzi ya Mungu.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na wasanii walioshinda Tuzo wakati wa hafla ya kumkabidhi Mhe Waziri Mkuu Tuzo za Filamu za Africa Magic Viewers Choice kutoka kwa wasanii Single Mtambalike (Richie) na Elizabeth Michael (Lulu) jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Rais wa Shirikisho la vyama vya Filamu Tanzania (TAFFA) Simon Mwakifamba, Profesa Elisante Ole Gabriel, Single Mtambalike, Elizabeth Michael, Naibu Waziri Mhe. Annastazia James Wambura na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania.
Baadhi ya wadau wafilamu wakifurahia wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Waziri Mkuu jana jijini Dar es Salaam.Tuzo hiyo ya Africa Magic Viewers Choice ambapo Filamu ya Kitendawili imeibuka kidedea kwa kuwa Filamu bora ya Kiswahili barani Afrika.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa  akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na wasanii wakati wa hafla ya kumkabidhi Mhe Waziri Mkuu Tuzo za Filamu za Africa Magic Viewers Choice kutoka kwa wasanii Single Mtambalike (Richie) na Elizabeth Michael (Lulu) jana jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Frank Shija, WHUSM)

No comments:

Post a Comment