Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli
Na Rose Masaka, MAELEZO
Dar Es Salaam, 13.08.2014
SERIKALI imetoa kiasi
cha Tsh. Bilioni 2.3 ya fidia kwa wakazi wa eneo la Mloganzila lililopo katika
Kijiji cha Kwembe Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam, ambao waliathiriwa
kutokana na ujenzi wa barabara kutoka Kibamba-Kisokwa hadi Barabara ya
Morogoro.
Akizungumza jana wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya Barabara katika Manispaa hiyo, Waziri
wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli alisema kwa mujibu wa vifungu vya sheria ya ardhi
na barabara inasema iwapo barabara ikimfuata mtu eneo alipo lazima mtu huyo
apewe fidia, na mtu atakayeifuata barabara hataweza kupewa fidia yoyote.
Kwa mujibu wa Dkt.
Magufuli aliongeza kuwa baadhi ya
wananchi waliokuwa wakiidai serikali tayari wamelipwa kulingana na madai yao,
na kuwa Serikali haipo kwa ajili ya kuonea watu na watu wasiionee serikali.
Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala
wa Barabara Tanzania Mhandisi Patrick Mfugale amesema kuwa katika awamu ya
kwanza ya mradi huo Serikali imekusudia kujenga barabara hiyo kwa urefu wa kilometa
4, meta 7 za upana pamoja na kutenga
eneo lenye ukubwa wa meta 4 kwa ajili ya waenda kwa miguu.
”Ujenzi ulianza mwaka
2013 mwezi wa 8, na kiasi cha Tsh. bilioni 6.4 zimetengwa kwa ajili ya
kukamilisha mradi huu na mradi huu wenye awamu mbili unatarajia kukamilika
mwaka 2016 na pia kiasi cha Tsh bilioni 1.6 zinatumika katika ajili ya utanuzi wa
barabara ya Kibamba yenye km 1.4” alisema Mfugale.
Katika hatua nyingine
Waziri Magufuli pia alifanya ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa mzani
eneo la Vigwaza uliopo Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani ambao unatarajiwa
kukamilika mwezi Septemba mwaka huu, ambapo mpaka kukamilika kwake unatarajia
kuigharimu Serikali kiasi cha Tsh. bil 10.11.
Dkt. Magufuli
aliwatahadhalisha madereva wa magari makubwa kuzingatia sheria za ujao wa
mizigo usiozidi uzito wa tani 56, kwani kitendo hicho cha kinaifanya Serikali
kutenga kiasi kikubwa cha fedha katika bajeti yake.
Katika Tanzania
asilimia 25 ya magari yanachangia kuharibika kwa barabara hizi tunazojijenga,
hivyo suala la kuzingatia sheria ya vipimo ni jambo muhimu kuzingatiwa na
madereva wote” alisema Waziri Magufuli.
Dkt. Magufuli alisema
mzani huo ni wa kisasa na Tanroad wanatakiwa kujifunza matumizi ya mtambo huo
kwa umakini na pia wanatakiwa kutoa mikataba maalumu kwa watumishi wa mzani huo
itakayoanisha hatua ya kinidhamu zitakazomkabili mfanyakazi huyo iwapo
kutatokea uharibifu wa makusudi wa mitambo katika mzani huo.


No comments:
Post a Comment