TANGAZO


Wednesday, May 1, 2013

SHIRIKA LA POSTA LAONYESHA UHAI WAKE MEI DEI MBEYA



WAFANYAKAZI WAKIWA  WAMEJIPANGA TAYARI KWA MAANDAMANO YA KUADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI 'MEI DEI' JIJINI MBEYA LEO. (PICHA ZOTE NA VENENCE MATINYA WA MBEYA YETU BLOG)
WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), WAKIPITA KWA MAANDAMANO MBELE YA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO HAYO KITAIFA, RAIS JAKAYA KIKWETE LEO.

GARI LA MAONESHO LA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA LIKIPITA KWENYE MAANDAMANO HAYO.
MOJA YA MAGARI YA MAONESHO YA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA LIKIPITA KUONESHA HUDUMA ZITOLEWAZO NA SHIRIKA HILO NCHINI NA NJE YA NCHI.
BAADHI YA WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA WAKIPITA KWA MAANDAMANO MBELE YA MGENI RASMI RAIS JAKAYA KIKWETE KATIKA MAADHIMISHO HAYO JIJINI MBEYA LEO.
LEONARD YEGELLA, MFANYAKAZI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), AKIPOKEA ZAWADI YA MFANYAKAZI BORA TOKA KWA RAIS KIKWETE KATIKA MAADHIMISHO HAYO.
MKOSA SHABAN MADANGANYA, AKIPOKEA ZAWADI KUTOKA KWA MWAKILISHI WA MKURUGENZI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), KATIKA HAFLA ILIYOFANYKA KATIKA UKUMBI WA MKAPA JIJINI MBEYA  LEO, MARA BAADA YA KUMALIZIKA MAANDAMANO HAYO LEO.
GENOVEVA ASSENGA, KARANI WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), MAKAO MAKUU DAR ES SALAAM, AKIPOKEA TUZO YA MFANYAKAZI BORA WA SHIRIKA
YEGELLA AKIPONGEZWA NA VIONGOZI WAKE.
MAGRETH MABULA, AKIPOKEA ZAWADI YA MFANYAKAZI BORA KUTOKA SHIRIKA LA POSTA, MKOA WA MBEYA
BAADHI YA WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA POSTA WAKISHANGILIA KWA FURAHA
AFISA UHUSIANO WA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), BWANA MIIGO AKIZUNGUMZA JAMBO WAKATI WA HAFLA YA KUWAPONGEZA WAFANYAKAZI BORA WA SHIRIKA HILO.
MENEJA WA SHIRIKA LA POSTA MKOA WA MBEYA HASSAN MWANG'OMBE AKIZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI (HAWAPO PICHANI) KATIKA HAFLA YA KUWAPONGEZA WAFANYAKAZI WAO.

WATUMISHI wa Umma na sekta binafsi nchini wameaswa kufanya kazi kwa bidii na kwa ushirikiano ili kuleta ufanisi katika kuziletea manufaa sekta wanazofanyia kazi.

Mwito huo umetolewa na baadhi ya Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania ambao wametunukiwa Zawadi za wafanyakazi bora kutokana na utendaji kazi wao baada ya kupigiwa kura na watumishi wenzao.

Wakizungumza wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na uongozi kwa wafanyakazi wote iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya baada ya kupewa nafasi ya kuwashukuru wenzao kwa kuwawezesha kuchaguliwa wafanyakazi bora wa Mwaka 2013.

Leonard Yegella (Principal Finance Officer- usimamizi)ambaye pia alitunukiwa zawadi ya mfanyakazi bora na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete alisema anafurahia kupewa nafasi kama hiyo ambayo ameipata kutokana na ushirikiano mzuri na wafanya kazi wenzie.

Wengine waliotunukiwa zawadi na Uongozi wa Posta ni pamoja na Bi Genoveva G. Assenga karani wa Posta kutoka makao makuu Dar Es Salaam, Bi. Magreth Mabula na Mkosa Shaban Madanganya walioibuka wafanyakazi bora kutoka Mkoa wa Mbeya.

No comments:

Post a Comment