TANGAZO


Sunday, May 19, 2013

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akutana na Wabunge wa CCM mjini Dodoma


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na Wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013 katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula. (Picha zote na Bashir Nkoromo).


Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula. 

Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.

Wajumbe kwenye kikao cha Mwenyekiti wa CCM na Wabunge wa CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.

Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.

Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya. 

No comments:

Post a Comment