Omar Al Somah alifunga bao kupitia mkwaju wa penalti dakika za mwisho na kuweka hai matumaini ya Syria kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018 kwa kutoka sare ya 1-1 na Australia.
Katika mechi yao ya awali, mshambuliaji Al Somah alifunga bao dakika za mwisho dhidi ya Iran na kulazimisha sare na iliyowawezesha kumaliza wa tatu katika kundi lao la kufuzu kwa Kombe la Dunia katika bara Asia.
Alifunga bao hilo la kusawazisha Alhamisi nchini Malaysia - ambapo Syria huchezea mechi zao za nyumbani - baada ya kuwa nyuma kutokana na bao la Robbie Kruse.
Mechi ya marudiano itachezwa Sydney Jumanne ijayo.
Mshindi atakutana na timu nyingine kutoka shirikisho la Concacaf kwenye mechi mbili (ya nyumbani na ya ugenini) kuamua timu itakayofuzu kwa Kombe la Dunia.
REUTERS


No comments:
Post a Comment