TANGAZO


Thursday, September 28, 2017

TANGAZO: MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI OKTOBA MOSI 2017 DODOMA, TANZANIA

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wanakukaribisha katika maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yatakayofanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Mjini Dodoma kuanzia Septemba 29 mpaka Oktoba 01,2017.

Mgeni Rasmi katika Maadhimisho haya atakuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili
Mhe. Ali Hassan Mwinyi.

Kauli Mbiu ni: “Kuelekea Uchumi wa Viwanda:Tuthamini Mchango, Uzoefu na Ushiriki wa Wazee kwa Maendeleo ya Taifa”

No comments:

Post a Comment