TANGAZO


Thursday, September 21, 2017

MAMIA WAMZIKA KAKA YAKE MUFTI WA TANZANIA,SHEHE SAAD ZUBEIRY ALLY

Waombolezaji wakiwemo ndugu, jamaa  na marafiki wakiwa wamebeba jeneza ambalo lina mwili wa  Kaka yake Mufti wa Tanzania, Sheikhe Saad Zubeiry Ally ambaye amefariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam wakijiandaa kuliingiza kaburini wakati wa mazishi yaliyofanyika jana (Septemba 21) kwenye makaburi ya familia eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe Mkoani Tanga.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir katika akizungumza wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika katika eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe Mkoani Tanga.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir (kulia), akiteta jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu wakati wa maziko ya kaka yake Mufti yaliyofanyika kwenye eneo la Makaburi ya familia eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Marry Chatanda.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto), akiteta jambo na
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira,January Makamba wakati wa maziko hayo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Makamba (kulia), akiteta jambo na Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam walipokutana msibani hapo wa kwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martin Shigella akiwa na mmoja kati ya waombolezaji katika msiba huo wakielekea makaburini.  
Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam kushoto akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku.
Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam akiondoka katika eneo la makaburini.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria mazishi hayo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia,Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe, Mhandisi Robert Gabriel wakiwa kwenye eneo la makaburini.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir kushoto akiwa na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku wakati wa mazishi hayo jana.
Sehemu ya waombolezaji katika msiba huo.
Shehe wa Mkoa wa Tanga,Juma Luwuchu akiwa katika eneo la msiba jana kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir akiagana na baadhi ya watu waliohudhuria mazishi ya kaka yake jana. 
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi waliohudhuria mazishi ya kaka yake kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu,Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandis Zena Saidi na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Marry Chatanda wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika akiwa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) mbele Marry Chatanda na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi. (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments:

Post a Comment