Pages

Thursday, August 10, 2017

Ajuza ambaye amehitimu shahada akiwa na miaka 91

Kimlan Jinakul

Haki miliki ya pichaPANUMAS SANGUANWONG/BBC THAI
Image captionKimlan alikuwa kati wa maelfu ya wale waliohitimu mwaka huu
Ajuza mweye umri wa miaka 91 kutoka nchini Thailand amepata shahada yake baada ya masomo yaliyomchukua karibu miaka 10.
Kimlan Jinakul amekuwa na ndoto wa kujiunga na chuo kikuu tangu awe mtoto lakini hakupata fursa hiyo.
Lakini miaka mingi baadaye baada ya kuwasomesha watoto wake hadi viuo vikuu, aliamua kujiunga na chuo na siku ya Jumatano amefanikiwa kupata shahada yake.
Kimlan Jinakul with familyHaki miliki ya pichaPANUMAS SANGUANWONG/BBC THAI
Image captionWatu wa famila yake walidhuria sherehe za kuhitimu kwake
Kimlan ambaye anatokea mkoa wa Lampang kaskazini mwa Thailand. Alikuwa mwanafunzi mwenye kuelewa masomo na alisomea kati ya shule bora zaidi mkoani humo.
Lakini hakufanikiwa kuendelea hadi chuo kikuu wakati huo na baada ya familia yake kuhamia mji wa Bangkok, aliolewa na kaachana na ndoto yake ya kusoma zaidi.
Watoto wake wanane kati ya watano wana shahada za uzamili na hata mmoja amefanikwa kupata shahada ya uzamifu au PhD nchini Marekani.
Juasiripukdee familyHaki miliki ya pichaKIMLAN JINAKUL
Image captionIlimchukua Kimlan zaidi ya miaka 10 kupata shahada
Wakati mmoja wa mabinti zakae ambaye alikuwa akifanya kazi hospitalini alianza kusoma katika chuo cha Sukhothai Thammathirat naye aliamua kujiunga.
Alikuwa na umri wa miaka 72 wakati alijiunga na chuo kiuu, lakini kufuatia kifo cha moja wa mabinti zake aliacha masomo kwa miaka kadha.
Akiwa na umri wa miaka 85 alirudi shuleni tena na kuendelea na masomo.

No comments:

Post a Comment