Hospitali nchini Kenya zimeanza kuwafuta kazi madaktari wanaogoma na kuwaondoa kutoka wa nyumba zao.
Huduma kwenye hospitali za umma zimetatizika kutokana mgomo ambao ulianza mwezi Disemba, huku madaktari na wahudumu wengine wa afya wakitaka mshahara zaidi na mazingira bora ya kufanya kazi.
Lakini hatua hiyo ya kuwafuta kazi madaktari inakuja wakati chama cha madaktari kinasema kuwa kimetia sahihi nyaraka zinazohitajika ili kumaliza mgomo wao.
- Madaktari Kenya wakataa nyongeza ya serikali
- Mahakama yawaagiza madaktari wanaogoma kurudi kazini Kenya
- Viongozi wa madaktari Kenya wafungwa jela
- Madaktari wapewa siku 5 kumaliza mgomo Kenya
- Kenya yapeleka madaktari wa jeshi kuhudumu hospitali za umma
Madaktari nao wanaitaka serikai kufanya hivyo.
Lakini serikali inasema kuwa siku ya mwisho ya kukubali asilimia 50 ya nyongeza ya mshahara ilipita siku mbili zilizopita.
Sasa hospitali zimeanza kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya madaktari ambao wamekuwa kwenye mgomo kwa siku 95.
No comments:
Post a Comment