TANGAZO


Tuesday, September 13, 2016

Viongozi wa nchi za IGAD kukutana mara ya kwanza Mogadishu

Mkutano wa Igad utafanyika chini ya ulinzi mkali

Image captionMkutano wa Igad utafanyika chini ya ulinzi mkali
Viongozi wa nchi wanachama wa muungano wa maendeleo Afrika Mashariki na pembe ya Afrika (IGAD) wanatarajiwa kukutana katika mkutano wa kihistoria mjini Mogadishu, Somalia.
Itakuwa mara ya kwanza kwa mkutano kama huo kufanyika mjini Mogadishu tangu kuanzishwa kwa muungano huo miaka 30 iliyopita.
Bango la kukaribisha washiriki wa mkutano huo
Image captionBango la kukaribisha washiriki wa mkutano huo
Wengi wa wanachama, Ethiopia, Uganda na Kenya, wamechangia wanajeshi katika kikosi cha walinda amani wa Umoja wa Afrika ambacho kinasaidia serikali kukabiliana na wanamgambo wa Kiislamu wa al-Shabab.
Mikutano kama hiyo haingeweza kufanyika katika mji huo kwa karibu mwongo mmoja uliopita kwa sababu za kiusalama.
Bendera za mataifa wanachama wa Igad
Image captionBendera za mataifa wanachama wa Igad
Mwandishi wa BBC aliyeko Mogadishu Ibrahim Aden anasema ulinzi mkali unadumishwa katika mji huo na barabara nyingi kuu zimefungwa.

No comments:

Post a Comment